Mkoa wa Kagera uko Kaskazini Magharibi mwa Tanzania Bara .Unapakana na nchi ya Uganda upande wa kaskazini, nchi za Rwanda na Burundi upande wa Magharibi, Mkoa wa Kigoma na Shinyanga kwa upande wa kusini na Mkoa wa Mwanza Kusini Mashariki.
KIKAO CHA KAMATI YA USHAURI CHA MKOA (RCC) 18/05/2010.
Kikao cha Ushauri cha Mkoa (RCC) kimefanyika tarehe 18/05/2010 katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na kuhudhuliwa na Viongozi mbalimbali wa Serikali, Wabunge, Viongozi wa Madhehebu ya Dini, Viongozi wa vyama vya Siasa na waandishi wa habari
Hapo juu ni picha ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mh. Mohamed Babu wakati anafungua kikao cha kamati ya ushauri cha Mkoa.
Kuanzia miaka ya tisini hadi sasa msukumo umekuwa ni kujenga mazingira mazuri ya utendaji serikalini ili kutoa huduma inayomjali mteja na kujenga utumishi wenye kuleta tija na ufanisi kazini