JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - OFISI YA MKUU WA MKOA KAGERA
     
 
     
 
 
     
BARABARA, MAWASILIANO NA UCHUKUZI
 
Barabara [ Majengo ] [ Nyumbani ] au
 
 

BARABARA

Mkoa wa Kagera unao mtandao wa barabara zenye urefu wa Km. 4785.66 zinazohudumiwa na Wakala wa Barabara (TANROADS) na Halmashauri za Wilaya/Manispaa.

Wakala wa Barabara (TANROADS)

Barabara zinazohudumiwa na Wakala wa Barabara (TANROADS) ni Km. 1840.2 ambazo zimegawanyika kama ifuatavyo :-

Na.

Aina ya barabara

Lami (Km)

1

Barabara za lami

397.8

2

Barabara za Changarawe

1,442.4

 

JUMLA KUU

1,840.2

Halmashauri za Wilaya/Manispaa

Barabara zinazohudumiwa na Halmashauri za Wilaya/Manispaa ni Km. 2,945.46 ambazo zimegawanyika kama ifuatavyo :-

Na.

Aina ya barabara

Lami (Km)

1

Barabara za lami

9.92

2

Barabara za changarawe

1,394.65

3

Barabara za udongo

1,540.89

 

JUMLA KUU

2,945.46

HALI YA BARABARA

Hali ya barabara kwa ujumla ni nzuri na karibu asilimia 90 ya mtandao wa barabara za mkoa huu zinapitika bila matatizo. Hali hii inatokana na Mkoa huu kuwa na miradi mingi ya barabara. Hata hivyo, baadhi ya barabara hasa zinazohudumiwa na Halmashauri ziko katika kiwango cha udongo na zinapitika kwa shida husasani kipindi cha mvua. Serikali imekuwa ikizifanyia matengenezo mbalimbali barabara hizo kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara (Road Fund) . Katika mwaka wa fedha wa 2007/08 Serikali imetenga jumla ya TShs. 6.96/= bilioni kwa matengenezo ya barabara za mkoa zinazohudumiwa na Wakala wa barabara (TANROADS) .

Fedha za matengenezo ya barabara za TANROADS

Na

Aina ya kazi

Malengo ya kazi

Fedha zilizoidhinishwa 2007/08

(Tshs. milioni)

1

Matengenezo ya Barabara kuu

Km. 467.26

 

3,641.957

Madaraja 126

2

Matengenezo ya Barabara za mkoa

Km. 1151.16

2,944.314

Madaraja 26

3

Miradi ya maendeleo katika barabara za mkoa kwa kiwango cha Lami

Km. 37

375.000

JUMLA

6,961.271

Na kiasi cha fedha Tshs.2.87/= bilioni kwa matengenezo ya barabara zinazohudumiwa na Halmashauri.

Fedha za matengenezo ya barabara za Halmashauri

Na

Aina ya kazi

Malengo ya kazi

Fedha zilizoidhinishwa 2007/08

(Tsh milioni)

1

Matengenezo ya kawaida

Km. 1833

1145.2

2

Matengenezo ya muda maalumu

Km. 100.94

1261.03

3

Matengenezo ya sehemu korofi

Km. 201.1

226.4

4

Ujenzi wa Madaraja/makaravati

Madaraja/makaravati

238.1

JUMLA YA GHARAMA

2,870.73

Karibu asilimia 25 ya bajeti ya barabara hizo imetumwa kwenye Halmashauri. Aidha, kwa kutumia wadau mbalimbali chini ya mpango wa STABEX jumla ya Km. 228.1 zimefanyiwa matengenezo kwa kiwango cha changarawe kwa gharama ya Tshs. 2.457/= bilioni. Kwa kutumia mfuko wa TASAF, mpango wa VTTP/LGTP na LGCDP , na wadau mbalimbali Mkoa umezifanyia matengenezo mbalimbali barabara za Halmashauri hususan maeneo ya vijijini.

HALI YA UTEKELEZAJI WA BARABARA KUU.

Mkoa unayo miradi ya ujenzi wa barabara kuu kwa kiwango cha lami ambayo imefikia katika hatua mbalimbali za utekelezaji. Mradi wa ujenzi wa barabara ya Kyamyorwa -Buzirayombo (Km. 120) kwa kiwango cha lami umefikia kiwango cha asilimia 99. Mradi wa ujenzi wa barabara ya Buzirayombo- Geita (Km 100) kwa kiwango cha lami umefikia asilimia 80, na ujenzi wa barabara ya Kagoma-Rusahunga (Km. 154) kwa kiwango cha lami umekwishaanza na maendeleo ya jumla ya mradi huu ni asilimia 10. Hata hivyo, kasi ya utekelezaji bado ni ndogo.

MATATIZO YA SEKTA YA BARABARA

•  Upungufu/Ukosefu wa Wakandarasi wenye uwezo na mitambo

•  Kulima/kujenga kwenye maeneo ya hifadhi ya barabara (Road reserve) .

•  Uharibifu/wizi wa alama za barabara (road sign)

•  Hali ya hewa hususan mvua nyingi ambayo huchangia kuharibu barabara.

•  Upungufu wa fedha (bajeti) za matengenezo ya barabara.

MKAKATI WA KUKABILIANA NA MATATIZO

•  Kutumia Mfuko wa kuinua Wakandarasi (CAF) ili kupata mikopo ya kununulia vifaa/mitambo ya ujenzi wa barabara.

•  Kutumia sheria n dogo ndogo (by-law) kulinda hifadhi ya barabara.

•  Kuomba fedha za kutosha kutoka kwenye Mfuko wa Barabara.

 

 

 

 
 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 

 

 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 
 
 

USAFIRI WA MAJINI

Mkoa wa Kagera hutegemea pia usafiri wa majini katika Ziwa Victoria. Meli za Shirika la Marine Tanzania (TMS) zimeendelea kutoa huduma ya usafiri wa mizigo na abiria kati ya miji ya Bukoba, Kemondo na Mwanza. Meli inayotoa huduma kwa sasa ni MV Serengeti na usafiri wa Boti ndogo. Hata hivyo, meli ya MV Victoria ambayo ni tegemeo kubwa kwa usafri wa abiria na mizigo kutoka Bukoba hadi Mwanza imekwama kwa zaidi ya miezi 6 kutokana na matengenezo. Hali hiyo imechangia usafiri kuwa mgumu.

Vile vile, Mkoa chini ya mpango wa POST OSAKA umejiwekea lengo la kurahisisha usafiri kutoka Bukoba kwenda Uganda kwa kujenga kivuko kitakacho unganisha Kata ya Kabango (Bukoba Vijijini) na mji wa Kasensero nchini Uganda . Mradi huu umetengewa bajeti ya Tshs. 400 mill. katika mwaka huu wa fedha. Kukamilika kwa mradi huu utasaidia kukuza uchumi kwa kusafirisha mazao ya biashara (export) , kuimarisha ushirikiano, kurahisisha mawasiliano na kupunguza uchakavu wa barabara.

MATATIZO YA USAFIRI WA MAJINI

•  Uchakavu wa gati katika bandari ya Bukoba na Kemondo Bay.

•  Uduni wa vyombo vya usafiri majini hususani meli na boti.

•  Upungufu wa kina cha maji kutokana na uharibifu wa mazingira.

MKAKATI WA KUKABILIANA NA USAFIRI MAJINI

•  Ukarabati wa Bandari na magati (routine maintenance) fedha za bajeti zinapopatikana.

•  Kuimarisha vyombo vya usafiri majini na kuhakikisha zina vifaa vya tahadhari (life jacket)

•  Utunzaji wa mazingira na vyanzo vya maji (environmental management) .

VIWANJA VYA NDEGE

Mkoa una kiwanja cha ndege kimoja. Mbali na kiwanja cha Bukoba, vipo viwanja vidogo 3 wilaya ya Ngara, Karagwe na Biharamulo ambavyo hutumiwa na ndege binafsi na kuimarishwa kwa ujenzi wa miundo mbinu na huduma nyinginezo. Kiwanja cha ndege cha Bukoba ambacho ni tegemeo kwa mkoa kina urefu wa Km. 0.9 , ambacho kutokana na ongezeko la abiria hakikidhi mahitaji. Mkoa unahitaji ndege kubwa zitakazoweza kuwahudumia wananchi na ili ndege hizo ziweze kutua katika uwanja huo unahitaji kuongezewa urefu wa zaidi ya Km. 0.3 na kufikia Km. 1.2 . Mkoa kwa kushirikiana na Wizara ya Miundo mbinu umekwisha kamilisha kazi ya upimaji, uthamini na upembuzi yakinifu (feasibility study) .

CHANGAMOTO/TATIZO

•  Gharama kubwa ya upanuzi na fidia (compensation) .

MKAKATI WA KUIMARISHA USAFIRI WA ANGA

•  Ujenzi wa kiwanja kikubwa cha kimataifa (international airport) katika eneo la Kajiunguti, Wilaya ya Missenyi.

MAWASILIANO YA SIMU

Kufuatia upanuzi wa mawasiliano ya simu kwa ujenzi wa mitambo mipya ya STD hapa mkoani, kumesaidia ongezeko la wateja kufikia 3,344. Mitandao ya mawasiliano ya huduma za simu za mkononi kupitia makampuni ya Mobitel, Vodacom, Celtel na Zantel imeenea katika miji yote ya makao makuu ya wilaya hadi maeneo ya vijijini.

 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
     
     
 
     
Copyright © 2008 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera, BUKOBA, TEL: 028 - 2220215/17, FAX: 028-2752184