JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - OFISI YA MKUU WA MKOA KAGERA
     
 
     
 
 
     
UGONJWA WA MNYAUKO BAKTERIA WA MIGOMBA
 
Title ya nyinginezo 5 [ Nyumbani ] au
 
UTANGULIZI
 

Ugonjwa huu hatari wa migomba unashambulia aina zote za migomba.Migomba iliyoshambuliwa hunyauka haraka na baadaye hufa kabisa.

Hapa Tanzania ugonjwa huu umeenea haraka na kuleta madhara katika wilaya za Muleba, Karagwe ,Biharamulo na Bukoba
Unaenezwa na bakteria aitwaye Xanthomonas campestris pv musaerum. Bakteria hao wana rangi ya njano ambayo hujitokeza kwenye utomvu mara shina la mgomba ulioathirika linapokatwa. Dalili za ugonjwa huo huonekana kwenye majani , ua dume, shina na mkungu

 

 
DALILI ZA UGONJWA
 
MAJANI
 
  • Majani hunyauka kama yaliyopitishwa kwenye moto na wakati mwingine hubadilika rangi na kuwa manjano.
  • Majani yaliyonyauka hayavunjiki kirahisi yakifikichwa ukilinganisha na yaliyokauka kwa jua au magonjwa mengine kama vile Panama.
  • Majani hupinda kuanzia katikati hadi nchani.Hii ni tofauti na majani ya migomba yaliyoshambuliwa na ugonjwa wa Panama ambayo hupinda jani linapoanzia.
 
SHINA
 

Shina linapokatwa hutoa utomvu wa njano. Baada ya muda mfupi utomvu huganda na kuwa kama kamasi.

 

 

MKUNGU
 
  • Ndizi huiva bila mpangilio kwenye mkungu
  • Ndizi zilizoiva huwa ngumu na zikimenywa hutoa harufu mbaya
  • Ndizi zikikatwa vipanda huwa na rangi nyeusi ndani.
  • Ndizi zilizoshambuliwa haziwezi kuliwa na viumbe kama nguruwe,ng'ombe, mbuzi na binadamu.
 
DALILI ZA UGONJWA KWENYE MKUNGU WA NDIZI
  • Kama dalili hazionekani , kata ndizi kutoka kwenye chane ya mwisho,na kama imeathirika itaonesha rangi nyeusi ndani.
  • Ndizi changa hunza kuiva kabla ya kukomaa.
 
ZINGATIA YAFUATAYO
 
Ukiona dalili zilizotajwa ,toa taarifa haraka kwa mtaalam wa kilimo au kwa kongozi yeyote wa serikali aliye karibu nawe kabla yakuchukua hatua zozote.
 
 
 
JINSI YA KUDHIBITI MNYAUKO BAKTERIA WA MIGOMBA
 

Ugomjwa huu unaweza kudhibitiwa kwa urahisi kama wakulima na wadau wengine watazingatia kanuni zilizotolewa.kanuni zeneywe ni rahisi kuzitekeleza kwa gharama nafuu.

 
 
 
NJIA KUUDHIBITI UGONJWA
 

Ondoa ua dume mara tu chane ya mwisho inapojitokeza ili kuzuia wadudu kama nyuki wasisambaze vimelea vya ugonjwa wakati wa kufyonza utomvu mtamu kutoka kwenye ua dume.

  • Ondoa ua dume kwa kutumia mti mkavu wenye panda.
  • Usitandaze maganda ya ndizi yaliyotoka nje ya shamba lako,bali yafukie shimoni.
  • Usitandaze takataka za migomba ambazo hufahamu zilikotoka.
  • Chimbua migomba iliyoathirika,ikatekate vipande vidogovidogo,irundike pamoja au chimba shimo na kuifukia. Usiendelee kuhudumia migomba mingine ambayo haijaathirika.
  • nawa mikono na safisha viatu vyako kwa kutumia mchanganyiko wa JIK na maji kwa uwiano wa 1 kwa 5 mara tu utokapo kuhudumia shamba lenye migomba iliyoathirika. Vilevile safisha vifaa vilivyotumika kukatakata mimea iliyoathirika kwa JIK au vipitishe katika moto.
  • Usiwaruhusu wafanyabiashara wa ndizi kutumia vifaa vyao kukata ndizi kwenye shamba lako.
  • Usiazime vifaa kama kisu,panga,chezo na chimbio na kuvitumia kwenye shamba lako.
  • Ukipanda miche ya migomba ambayo hufahamu inapotoka maana inaweza kueneza ugonjwa.
  • Panda miti iliyothibitika kutokuwa na ugonjwa wa mnyauko bakteria wa migomba.
  • Usisafirishe ndizi, miche au majani ya migomba kutoka maeneo yenye ugonjwa.
  • Toa taarifa kwa mtaaalam wa kilimo au kwa kiongozi yeyote wa Serikali aliye karibu nawe mara tu uonapo dalili za ugonjwa huu mahali popote.
 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 
[ Nyumbani ] au
Rudi juu
 
     
Copyright © 2008 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera, BUKOBA, TEL: 028 - 2220215/17, FAX: 0282752184