JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - OFISI YA MKUU WA MKOA KAGERA
     
 
     
BKBVIJIJINI
 
 
     
HALMASHAURI YA WILAYA YA BUKOBA VIJIJINI
 
Halmashauri < [ Nyumbani ] au
 
 

ELIMU

 

Elimu ya Awali

 

Shule za Awali zilizopo ni 138 zenye jumla ya wanafunzi 7,918 MV 3,940 na WS 3,978; Mahitaji halisi ya Shule hizo ni 143. Mkakati ni kuhakikisha kila Shule ya Msingi ina darasa la awali.

 
 

•  Elimu ya Msingi

 

Kuna jumla ya Shule za Msingi 143 Serikali 140, binafsi 3, Wanafunzi walioko shuleni kwa mwaka huu 2008 ni 66,353. Kati ya hao wavulana ni 33,041 (49.7.%) na wasichana ni 33,310 (sawa na 50.3%). Kuna vyumba vya madarasa 922 wakati mahitaji halisi ni vyumba 1,547. Hivyo kuna upungufu wa vyumba vya madarasa 625 (41%). Wapo Walimu 1,325 ukilinganisha na mahitaji ya Walimu 1,659. Uwiano wa Wanafunzi kwa chumba cha darasa ni 1:50.

Lengo la uandikishaji Mwaka 2007 ni wanafunzi 8,759 (wavulana 4,497 na wasichana 4,262). Walioandikishwa walikuwa ni jumla ya wanafunzi 8741 wakiwa wavulana 4488 na wasichana 4253 sawa na asilimia 99.8.

 
 

Ongezeko la Mahitaji ya Huduma ya Elimu Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba.

 

NA

 

HUDUMA

 

MAHITAJI

 

YALIYOPO

 

UPUNGUFU/

ZIADA

1

Nyumba za Walimu

1,546

227

1,319

2

Vyumba vya Madarasa

1,547

922

625

3

Madawati

32,849

23,225

9,624

4

Matundu ya Vyoo

2,850

1,091

1,759

5

Walimu

1,703

1,325

378

 
 

 

  Vyuo vya Ufundi

Vyuo vya Ufundi vilivyopo ni 1 kati ya hivyo 1 ni cha Serikali na 3 ni vya binafsi. Kuna wanafunzi 21 (Me 7 na Ke 14) walioandikishwa.

 

Elimu ya Watu Wazima

 

Vipo Vituo 336vya kisomo vyenye jumla ya wanafunzi 5,138. Kati ya hao 2,329 ni wanaume na 2,809 ni wanawake. Elimu ya Watu Wazima inakabiliwa na tatizo la mahudhurio duni, viwango vidogo vya malipo ya Walimu wa Kisomo, upungufu wa vifaa na vitendea kazi. Vile vile Vituo 60 vya MEMKWA vimeanzishwa vikiwa na wanafunzi 366 sawa na wavulana 182 na wasichana 184

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 
 
 
Hatua zilizochukuliwa kuondoa upungufu huu:
 

•  Kuendelea kurekebisha mgawanyo wa Walimu katika Shule za Msingi ili uzingatie idadi ya wanafunzi kwa kila shule, na kuajiri walimu wapya kuondoa upungufu, kwa nia hiyo walimu 51 wameajiriwa.

•  Kuendelea kuhimiza kila Kamati za maendeleo ya kata kuandaa mikakati wa kuchangia utengenezaji wa madawati na samani zingine kulingana na mahitaji, kwa lengo la kumaliza upungufu uliopo.

•  Kusimamia kwa ukamilifu utekelezaji wa Mpango wa MMEM na Uboreshaji wa Elimu.

•  Kuendelea kushirikiana na Wadau mbalimbali kama World Vision, n.k; ili kusaidia uboreshaji wa Sekta hii ya Elimu.

 

 
 
 
Elimu ya Sekondari
 

Zipo shule 28 ambazo kati ya hizo 24 ni za Serikali na 4 zinamilikiwa na watu binafsi na zisizo za Kiserikali. Kuna jumla ya wanafunzi 7,719 kati ya hao wasichana ni 3,525 (sawa na 46.0%) na wavulana ni 4,194 (sawa na 54.0%).

Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Sekondari hizo mwaka 2007 ni kama ifuatavyo:-

Jedwali Na. 4 – Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga na Sekondari kwa Halmashauri ya Wilaya Bukoba .

HALMASHAURI YA WILAYA BUKOBA .

 

WAV

 

WAS

 

Jumla

 

Asilimia

  Waliofanya mtihani

2,057

2,299

4,806

86.8 %

 

 

 

 

 

  Waliofaulu

1,857

1,517

3,378

70.2%

 

 

 

 

 

  Waliochaguliwa

1,857

1,517

3,378

100%

Hatua kadha zinachukuliwa ili kukabiliana na upungufu wa wanafunzi wanaojiunga na Sekondari ni pamoja na:-

•  Kuihamasisha Sekta Binafsi/Taasisi kuwekeza katika Elimu ya Sekondari.

•  Kuanzisha ujenzi wa shule mpya za kutwa katika ngazi za Kata kwa kushirikisha jamii kuchangia nguvu, fedha na vifaa.

•  Kuendelea kushirikisha Wadau wengine wa Elimu ili kukarabati majengo na kujenga majengo mapya ya Sekondari za kutwa zilizoanzishwa.

•  Kuhakikisha kila Kata wanajenga shule moja ya Sekondari ya wananchi.

•  Kuendelea kusimamia kwa ukamilifu utekelezaji wa mpango wa uboreshaji wa Elimu ya Sekondari (MMES).

 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
     
     
 
     
Copyright © 2008 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera, BUKOBA, TEL: 028 - 2220215/17, FAX: 027-2752184