Katika kutekeleza azma ya Serikali ya kupiga vita umasikini miongoni mwa jamii ya Watanzania, Vijana na Wanawake wamepewa kipaumbele kwa kuendeleza miradi yao ama katika makundi yao au mmoja mmoja. Halmashauri imetoa mikopo kwa vikundi vya Wanawake.
Jumla ya Tshs. 33,482,481.50 zimetolewa kwa vikundi 33 vya wanawake na vijana. Mikopo hiyo inatoa taathira nzuri kwa vikundi hivyo kwani urejeshaji wake unaridhisha. Jumla ya Tshs. 21,482,481.50 zimerejeshwa na wahusika kiasi kilicho bado kurejeshwa muda wake wa kurejeshwa haujafika. |