JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - OFISI YA MKUU WA MKOA KAGERA
     
 
     
BKB VIJ
 
 
     
HALMASHAURI YA WILAYA YA BUKOBA VIJIJINI
 
Halmashauri < [ Nyumbani ] au
 
 
 

  MIFUGO

 

Ufugaji ni moja ya Sekta muhimu katika uchumi wa Wilaya yetu. Sekta hii inasaidia na kutegemewa sana katika:-

•  Kilimo (urutubishaji).

•  Chakula (Lishe).

•  Biashara (Mazao yake kama nyama, ngozi, mifugo yenyewe).

•  Aina mbili za ufugaji zinatumika Wilayani hapa ambazo ni ufugaji huria na ufugaji wa ndani. Wananchi wetu hasa wa Vijijini kwa asili ni wafugaji huria. Ufugaji huria umetengewa hekta 660 kwa ajili ya malisho. Pamoja na uendelezaji wa ufugaji huu, juhudi za kuwahamasisha wakulima na wafugaji kupanua ufugaji wa ndani zinafanywa. Mashirika mbalimbali Mfano; World Vision imeendesha mpango wa kutoa mafunzo ya ufugaji ng'ombe wa maziwa na kuwakopesha wakulima/wafugaji ng'ombe wa maziwa.

Wakulima na Wafugaji wetu wanapata huduma ya kinga na tiba kwa kushirikiana na Wataalam wa Mifugo. Magonjwa makuu ya mifugo ni minyoo, ndigana kali, ndigana baridi na kichaa cha mbwa.

Zifuatazo ni takwimu za mifugo Wilayani:-

NA

AINA YA MFUGO

IDADI

1.

Ng'ombe wa Asili

Ng'ombe wa Maziwa

30,272

2,769

2.

Mbuzi wa Asili

Mbuzi wa Maziwa

66,226

735

3.

Kondoo

5,686

4.

Nguruwe

1,277

5.

Kuku wa Asili

74,560

6.

Bata

6,025

7.

Mbwa

4,795

 

 

 

 

 

 
 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 

 

 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
     
     
 
 
 
     
Copyright © 2008 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera, BUKOBA, TEL: 028 - 2220215/17, FAX: 027-2752184