KUONDOA KERO ZA WANANCHI NA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA
Kero na vitendo vya rushwa ni mambo yanayosababisha chombo au Serikali yeyote ichukiwe sababu ya kutokuwepo haki. Kama ilivyoainishwa katika Ilani ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2000. Halmashauri imeendesha shughuli zake zikilenga kuondoa kero za wananchi na kupunguza au kuondoa kabisa mianya ya rushwa kwa njia zifuatazo:-
Taarifa za mapato na matumizi huwa wazi kwa umma.
Taratibu za ajira wakati wote zinazingatia miongozo na sheria.
Mipango ya maendeleo imeweka kipaumbele matakwa na inajibu hoja za wananchi mfano wake ni:-
Ujenzi wa madarasa.
Miradi ya kilimo na ufugaji.
Uimarishaji Vyama vya Ushirika ili viweze kutenda kazi kwa uwazi.
Mabaraza ya Kata yameundwa ili kusuluhisha migogoro miongoni mwa wananchi.
Halmashauri imeweka masanduku ya maoni ili kuwawezesha wananchi kutoa maoni yao na malalamiko yao na yanafanyiwa kazi kwa huandikwa kwenye rejista ya maoni ambayo hukaguliwa chini ya Mpango wa uboreshaji wa Serikali za Mitaa (yaani ni kigezo cha utawala bora)
Uendeshaji wa shughuli zote kwa njia za vikao:-
Baraza la Madiwani hutangazwa na huwa wazi kwa watu wote.
Mikutano Mikuu ya Mitaa/Vijiji hujadili kwa uwazi mambo yote yahusuyo maisha yao.
Vikao vya Mitaa/Vitongoji hutoa pia nafasi kwa wanavijiji kujadili kwa uwazi. Mambo yote yahusuyo maendeleo na maisha yao.
Vikao vingine kama vile Kamati za Kudumu za Madiwani, Wakuu wa idara, Serikali za Vijiji na Mikutano ya Mradi mbalimbali kama vile ya “World Vision (T)”, Columbia Universty, TADEPA, n.k. hutoa nafasi za wahusika kwa niaba ya wale wanaowawakilisha
|