JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - OFISI YA MKUU WA MKOA KAGERA
     
 
     
BKB MAN
 
 
 
HALMASHAURI YA MUNISPAA BUKOBA
 
[ Nyumbani ] au
 
AFYA:
 
UTANGULIZI
 

Halmashauri ya Mji wa Bukoba ni moja kati ya Halmashauri sita za Serikali za Mitaa zilizopo katika Mkoa wa Kagera. Halmashauri hii ilianzishwa wakati wa utawala wa Kiingereza chini ya Sheria ya “Local Government Ordinance” Cap 333 tarehe 27 Juni 1960 . Halmashauri hii ilianzishwa tena kama Halmashauri ya Mji chini ya Sheria ya “The Local Government Act” Namba 8 ya mwaka 1982 baada ya kufutwa kwa Serikali za Mitaa mwaka 1972 kutokana na Sheria ya Madaraka Mikoani.

Kwa sasa Bukoba ni mojawapo kati ya halmashauri 8 za Miji zilizotangazwa kupanda hadhi na kuwa Manispaa kama zilivyotangazwa katika gazeti la Serikali Na. 219 la tarehe 29/07/2005 .

 

 
 
 
 

•  Kijiografia

 

Halmashauri ya Mji wa Bukoba ipo upande wa kaskazini mashariki ya mkoa wa Kagera. Halmashauri hii ni moja kati ya Halmashauri mbili zinazounda wilaya ya Bukoba. Halmashauri ya Mji ipo katika latitudo 1 0 6'-1 0 8' 42” kusini kidogo tu ya mstari wa Ikweta na kati ya longitudo 31 0 16' 12” na 31 0 18'54” mashariki ya mstari wa Greenwich .Ipo mita 1,100 juu ya usawa wa bahari. Hali hii inafanya Halmashauri kuwa na misimu miwili ya mvua yaani vuli ambayo huanza Septemba na kumalizika Desemba na masika ambayo huanza Machi na kumalizika Juni. Kipindi cha Julai hadi mwanzoni mwa Septemba ni kiangazi na kipupwe huanza Januari hadi Februari. Halmashauri ya Mji inapakana kwa upande wa mashariki na Ziwa Victoria na pande zingine zote imezungukwa na Halmashauri ya wilaya ya Bukoba . Wastani wa mvua kwa mwaka ni milimita 1200 ambazo hufanya mimea kuwa na umbijani kwa mwaka mzima.

 

 
 
 

  Eneo

 

Halmashauri ya Mji wa Bukoba ina ukubwa wa kilometa za mraba 80 kati ya hizo, kilometa za mraba 22 (27.5%) zimefunikwa na maji hasa ya Ziwa Victoria na eneo lilobaki la kilometa za mraba 58 (72.5%) ni nchi kavu. Kimkoa eneo la Mji wa Bukoba ni sawa na 0.28% ya eneo lote la mkoa wa Kagera ambalo ni kilometa za mraba 40,838. Eneo linalofaa kwa kilimo ni Ha 42,000 wakati eneo linalolimwa kwa sasa ni Ha 3,860 tu. Jumla ya Ha 168.4 zimepandwa miti na maua ya aina mbali mbali.

 

 

 

 

 

 

 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 
 
 

Utawala

 

Halmashauri ya Mji ina Tarafa 1 ya Rwamishenye yenye Kata 14 na mitaa 66. Kati ya Kata hizo, Kata 8 zipo kijijini, na 6 zina mazingira ya kimji.

 

 
 
 

Uwakilishi wa wananchi

 

M A D I W A N I

WABUNGE

 

MADIWANI WA KATA

 

VITI MAALUM

MBUNGE WA JIMBO

 

VITI MAALUM

14

5

1

3

CCM

CUF

TLP

CCM

CUF

TLP

CCM

CCM

CUF

10

3

1

3

1

1

1

2

1

 

 
Idadi ya watu
Kulingana na sensa ya watu na makazi ya mwaka 2002, kuna watu wapatao 81,221. Kati ya hao, 40,822 (50.3%) ni wanaume na 40,399 (49.7%) ni wanawake. Msongamano wa watu ni 1,400 kwa kila kilometa moja ya mraba ya nchi kavu (yaani kilometa za mraba 58) ukilinganisha na takwimu za mkoa ambazo ni watu 47 kwa kila kilometa moja ya mraba. Ongezeko la watu kwa mwaka ni 4 %.
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
     
     
 
     
Copyright © 2008 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera, BUKOBA, TEL: 028 - 2220215/17, FAX: 027-2752184