Idara ya afya hutoa huduma za kinga na tiba katika kipindi chote cha mwaka kwa kutekeleza shughuli mbalimbali jinsi zilivyopangwa katika mpango wake wa mwaka.
Huduma hizi hutolewa kupitia jumla ya Vituo vya huduma 34 ambavyo ni pamoja na:-
Hospitali 3 za Rubya (Hospitali Teule ya Wilaya), Ndolage na Kagondo, zote za Mashirika ya Kidini.
Vituo vya Afya vya Kaigara na Kimeya.
Zahanati 29 ambazo ni:
i) 19 za Serikali
ii) 6 za mashirika ya dini
iii) 2 za Taasisi za serikali
iv) 2 za Binafsi
|