Wilaya inapakana na Wilaya ya Bukoba upande wa Kaskazini, Magharibi inapakana na Wilaya ya Karagwe, Kusini inapaka na Wilaya ya Biharamulo, Kusini Mashariki inapakana na Wilaya ya Chato na Mashariki inapakana na Mkoa wa Mwanza.
Wilaya ina eneo la kilomita za mraba 10,739 na kati ya hizo kilomita za mraba 3,444 ni nchi kavu na kilomita za mraba 7,295 ni eneo la maji hususani Ziwa Victoria . Eneo la nchi kavu linahusisha pia zaidi ya visiwa ishirini vilivyomo katika Ziwa Victoria .
JIOGRAFIA YA WILAYA
Wilaya ya Muleba imetawaliwa na vilima, mabonde na tambarale (plateaus). Wilaya ipo kati ya mwinuko wa mita 1,150 na 1,667 kutoka usawa wa bahari na sehemu ya juu kabisa ni Karambi. Mto Ngono unakatisha wilaya kuanzia Kusini kuelekea Kaskazini ambapo unaungana na Mto Kagera unaomwaga maji yake katika Ziwa Victoria.
Wilaya imegawanyika katika kanda kuu nne za kilimo ambazo ni: Ukanda wa mwambao wa Ziwa na Visiwa katika Ziwa Victoria, Ukanda wa juu, Ukanda wa chini Kusini na Ukanda wa Burigi. Ukanda wa mwambao wa Ziwa na ukanda wa juu unapata kipindi kirefu cha unyevunyevu (miezi 8 – 9) wakati ukanda wa chini na wa Burigi unapata kipindi cha unyevunyevu cha miezi 3 – 4 tu kwa mwaka.
Mvua zinanyesha zaidi upande wa Kaskazini – Mashariki yaani milimita 1800 wakati Kusini – Magharibi ni pakame. Kwa kufuata viwango vya miinuko na mvua, Wilaya inakuwa na kanda za kilimo tofauti zenye mazao mbali mbali yanayopandwa katika misimu tofauti.
Hali ya rutuba ya udongo si ya kuridhisha hasa kutokana na mvua nyingi zinazosababisha kuondolewa kwa virutubisho udongoni. Hata hivyo maeneo ya mabonde ya upande wa Kusini – Magharibi na miinuko tambarale (plateaus) yana rutuba ya kutosha wakati maeneo ya mwambao wa ziwa hayana rutuba.
IDADI YA WATU
Kulingana na takwimu za sensa ya watu na makazi za mwaka 2002 na ongezeko la watu la asilimia 2.5 kwa mwaka wilaya kufikia mwaka huu wa 2008 inakadiriwa kuwa na jumla ya watu wapatao 453,931 na kati ya hao watu 225,891 ni wanaume na watu 228,039 ni wanawake.
Msongamano wa watu kwa kilomita ya mraba ni 110. Watu wenye uwezo wa kufanya kazi ni asilimia 24 ya watu wote wakati watu wenye umri wa kwenda shule ni asilimia 30, zipo kaya 81,084 na wastani wa watu katika kaya ni 4.7.
Jedwali Na.1, 2 na 3 hapa chini vinachambua kwa kina takwimu za sensa ya watu na makazi ya mwaka 2002 kama ifuatavyo:-
Jedwali Na. 1 : Idadi ya watu kwa umri na jinsi
Umri |
Me |
Ke |
Jumla |
0 -1 |
29718 |
32219 |
61937 |
1 – 5 |
29860 |
30760 |
60620 |
6 – 14 |
31518 |
28519 |
60037 |
15 – 24 |
34951 |
33697 |
68648 |
25 – 44 |
29331 |
25584 |
54915 |
45 – 60 |
19971 |
22957 |
42928 |
60+ |
16903 |
20340 |
37243 |
Jedwali Na. 3: Mlinganisho wa jinsi katika Grafu

Jedwali Na. 3: Idadi ya watu Kitarafa.
Tarafa |
Idadi ya Kata |
Idadi
ya vijiji |
Idadi ya Mitaa |
Me |
Ke |
Jumla |
Muleba |
6 |
22 |
2 |
27354 |
27760 |
55114 |
Izigo |
6 |
25 |
|
9123 |
8893 |
18016 |
Kamachumu |
4 |
15 |
|
29988 |
30759 |
68648 |
Nshamba |
9 |
39 |
|
72769 |
73398 |
146167 |
Kimwani |
6 |
31 |
|
53018 |
53266 |
106284 |
Total |
31 |
132 |
2 |
192252 |
194076 |
386328 |
UTAWALA NA UONGOZI KISIASA
KIUTAWALA
Kama ilivyoonyeshwa kwenye jedwali Na. hapo juu wilaya ya Muleba imegawanyika katika Tarafa tano (5) nazo ni Izigo, Kamachumu, Muleba, Nshamba na Kimwani. Tarafa hizo tano nazo zimegawanyika katika kata 31, vijiji 132, mitaa 2 na vitongoji 677.
KISIASA
Wilaya pia imegawanyika katika majimbo mawili ya uchaguzi. Jimbo la Muleba Kusini linaongozwa na Mh. Anna Tibaijuka (Mb) na Jimbo la Muleba Kaskazini linaongozwa na Mh. Mwijage (MB), na wote wawili wanatoka Chama Tawala cha CCM.
Upande wa Kata, Kata zote 30 zinao madiwani wa kuchaguliwa ambapo kata moja iko wazi baada ya diwani wake kufariki dunia na Kata 2 madiwani wake ni wa kutoka kambi ya upinzani. Madiwani hawa wote ni wanaume. Wapo pia madiwani 11 wanawake wa viti maalum ambapo 8 ni wa kutoka chama cha CCM na 3 wanatoka kwenye vyama vya TLP 1 na CUF 2. |