Kwa kuzingatia kuwa ushirika ni chombo muhimu katika ujenzi wa uchumi endelevu na kuondoa umaskini, wananchi wanajianzishia vikundi vya ushirika vya uzalishaji mali vilivyo huru. Wilaya imekuwa ikijihusisha na uhamasishaji wa uzalishaji, uendelezaji na uimarishaji wa vikundi mbalimbali vya ushirika.
Idadi ya vyama vya ushirika hapa wilayani ni 136 na vimegawanyika kama ifuatavyo:
i) Vyama vya Ushirika vya mazao ..............50
ii) Vyama vya Kuweka na Kukopa ..............51
iii) Vyama vya Uvuvi ..................................5
iv) Vyama vya Mifugo ................................5
v) Vyama vya Kilimo .................................7
vi) Vyama vya Kibenki .............................16
vii) Chama cha Ushirika cha Mazingira......... 1
viii) Chama cha ushirika cha usafirishaji...... 1
Jumla...................................................136
|