JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - OFISI YA MKUU WA MKOA WA KAGERA
     
 
     
MULEBA
 
 
     
HALMASHAURI YA WILAYA YA MULEBA
 
Halmashauri < [ Nyumbani ] au
 
 
 
BARABARA
 

Walaya ya Muleba inazo barabara zenye urefu wa kilomita 1103 nyingi zikiwa za udongo na changarawe kama jedwali namba 4 linavoonyesha hapa chini.

Aina za barabara.

Na

Aina ya barabara

Urefu km.

Asilimia

1.

Barabara kuu

103 km

9

2.

Barabara za mkoa

175 km

15

3.

Barabara za Wilaya

210 km

19

4.

Barabara za vijiji

615 km

57

 

Jumla

1103 km

100

Barabara hizi kwa ujumla si mbaya sana , lakini kutokana na mmomonyoko wa udongo unaotokana na wingi wa mvua zinazonyesha kati ya mwezi Septemba hadi Desemba na Machi hadi Mei zinahitaji matengenezo ya mara kwa mara. Kikwazo kikubwa ni uhaba wa fedha za kuboresha barabara hizi.

Mpango wa Taifa wa kutengeneza barabara kwa kiwango cha lami tayari umeonyesha matunda ambapo barabara ya Mtukula – Bukoba – Kagoma (Muleba) tayari imejengwa kwa kiwango cha lami.

Pia barabara kutoka Kyamyorwa hadi Chato imeshatengenezwa kwa kiwango cha lami. Aidha ujenzi wa barabara kuanzia Kagoma kwenda Rusahunga kupitia Biharamulo umekwishaanza japokuwa kwa sasa umesimama.Matarajio yetu ni kwamba mradi huo utaendelea hivi karibuni.

•  Usafirishaji wa abiria na mizigo

Usafiri wa abiria na usafirishaji wa mizigo hutegemea sana magari kwa nchi kavu na mitumbwi kwa upande wa majini. Vyombo vyote hivi humilikiwa na watu binafsi. Hatuna usafiri wa anga kwa kuwa hatuna uwanja wa ndege, isipokuwa. kuna uwanja mdogo wa ndege kwa ajili ya ‘'Flying Doctors'' kwa hospitali teule ya wilaya (Rubya).

 

 

 
 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 

 

 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
     
     
 
 
 
     
Copyright © 2008 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera, BUKOBA, TEL: 028 - 2220215/17, FAX: 028-2752184