Kuumwa na mbwa wenye kichaa.
Uti wa mgongo.
Homa ya matumbo.
Kuhara damu.
Magonjwa ya watoto.
UKIMWI.
Elimu ya Afya inaendelea kutolewa kwa wananchi ili wajikinge na magonjwa haya. Kuna mafanikio makubwa katika magonjwa mengine isipokuwa Ugonjwa wa Ukimwi ambao bado ni tishio kwa wananchi wetu. Juhudi zaidi zinahitajika ili kufanya jamii iweze kubadili tabia.
Hali ya Ukimwi Wilayani
Hali ya Ugonjwa wa UKIMWI katika Wilaya ya Missenyi – Maambukizi:-
Kwa ujumla hali ya maambukizi ya HIV/AIDS katika Wilaya inaonyesha kuongezeka. Sawia na kuongezeka kwa ugonjwa wa UKIMWI kuna ongezeko kubwa la magonjwa ya zinaa jambo linaloonesha kwamba jamii bado haijabadili tabia kwa kufanya ngono salama.
Matokeo ya vipimo vya damu yanaonesha kiwango cha maambukizi kupungua na kuongezeka kila mwaka. Kiwango cha maambukizi ya HIV/AIDs katika Wilaya kwa mwaka 2007 kilikuwa wastani wa 3.3% na Kwa mwaka 2008 kiwango cha maambukizi kimefikia 5.9% kufuatia takwimu za VCT 7%, PMTCT(4.8%) na Wanaojitolea damu.( 0%)
Mikakati ya Kupambana na UKIMWI
Kuendelea kutoa elimu shuleni, vyuoni na Jamii nzima
Kuhamasisha jamii kupima Afya zao na kubadili tabia.
Kuimarisha kampeni ya Ishi ambayo imeanzishwa wilayani.
Kutoa elimu kuhusu UKIMWI katika sehemu za kazi.
Kutoa elimu kwa wafanyakazi wa baa, mahoteli na nyumba za kulala wageni,
Kushirikisha na kushirikiana na madhehebu ya dini ili kutoa elimu kwa waumini wa madhehebu mbalimbali.
Kuanzisha na kuimarisha Kamati za UKIMWI za Wilaya, Kata na Vijiji/Vitongoji.
Kuelimisha jamii kufanya ngono salama kwa kuhimiza matumizi ya kondomu kwa usahihi, kwa kutumia vikundi vya sanaa na mikutano ya hadhara. |