JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - OFISI YA MKUU WA MKOA KAGERA
     
 
     
MISENYI
 
 
     
HALMASHAURI YA WILAYA YA MISSENYI
 
Halmashauri < [ Nyumbani ] au
 
 
 
ELIMU
 

Elimu ya Awali

Shule za Awali zilizopo ni 94 zenye jumla ya wanafunzi 4,909 Me 2,451 na Ke 2,458 shule zote za msingi zina madarasa ya awali

Elimu ya Msingi

Kuna jumla ya Shule za Msingi 97 zikiwemo 94 za Serikali na 3 za binafsi/mashirika ya dini. Wanafunzi walioko shuleni kwa mwaka huu 2009 ni 40,102 Kati ya hao wavulana ni 20,309 (51%) na wasichana ni 19,793 (sawa na 49%). Idadi ya mikondo imeongezeka kutoka mikondo 888 mwaka 2007 hadi mikondo 891 mwaka 2009. Idadi ya wanafunzi wanaojiunga na elimu ya sekondari imeongezeka kwa asilimia 23.24 kutoka wanafunzi 2,246 mwaka 2007 hadi kufikia 2,768 mwaka 2008

Ongezeko la Mahitaji ya Huduma ya Elimu ya Msingi Halmashauri ya Wilaya ya Missenyi.

 

NA

 

HUDUMA

 

MAHITAJI

 

YALIYOPO

 

UPUNGUFU/ ZIADA

1

Nyumba za Walimu

933

197

736

2

Vyumba vya Madarasa

943

616

327

3

Madawati

20612

14404

6208

4

Matundu ya Vyoo

1692

735

957

5

Walimu

891

794

97

Chanzo: Idara ya Elimu, 2009

Hatua zilizochukuliwa kuondoa upungufu huu:-

•  Kujenga madarasa 327 Madarasa 20 yanaendelea kujengwa.

•  Kuendelea kurekebisha mgawanyo wa Walimu katika Shule za Msingi ili uzingatie idadi ya wanafunzi kwa kila shule, na kuajiri walimu wapya kuondoa upungufu, kwa nia hiyo walimu 27 wameajiriwa.

•  Kuendelea kuhimiza Kamati za maendeleo za kata kuandaa mikakati wa kuchangia utengenezaji wa madawati na samani zingine kulingana na mahitaji, kwa lengo la kumaliza upungufu uliopo.

•  Kusimamia kwa ukamilifu utekelezaji wa Mpango wa MMEM na Uboreshaji wa Elimu.

•  Kuendelea kushirikiana na Wadau mbalimbali kama World Vision, Kagera Sugar na Partage ili kusaidia uboreshaji wa Sekta hii ya Elimu.

 

 

 

 
 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 

 

 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 
 
 
 
 

Elimu ya Sekondari

Zipo shule 21 ambazo kati ya hizo 18 ni za Serikali na 3 zinamilikiwa na watu binafsi/Mashirika ya dini. Kuna jumla ya wanafunzi 7,465 kati ya hao wasichana ni 3,567 (sawa na 48%) na wavulana ni 3,897 (sawa na 52%). Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Sekondari mwaka 2009 ni kama ifuatavyo:-

WALIOFAULU

WAV

WAS

Jumla

Asilimia

1487

1481

2968

100

WALIOCHAGULIWA

WAV

WAS

Jumla

 

1487

1481

2968

100

Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga na Sekondari kwa Halmashauri ya Wilaya Missenyi

Chanzo: Idara ya Elimu, 2009

Hatua kadha zinachukuliwa ili kukabiliana na upungufu wa wanafunzi wanaojiunga na Sekondari nazo ni:-

•  Kuihamasisha Sekta Binafsi/Taasisi kuwekeza katika Elimu ya Sekondari.

•  Kuanzisha ujenzi wa shule mpya za kutwa katika ngazi za Kata kwa kushirikisha jamii kuchangia nguvu, fedha na vifaa.

•  Kuendelea kushirikisha Wadau wengine wa Elimu ili kukarabati majengo na kujenga majengo mapya ya Sekondari za kutwa zilizoanzishwa.

•  Kuhakikisha kila Kata wanajenga shule moja ya Sekondari ya wananchi.

•  Kuendelea kusimamia kwa ukamilifu utekelezaji wa mpango wa uboreshaji wa Elimu ya Sekondari (MMES).

•  Kuaanda mazingira ya kuendesha na kusimamia Elimu ya sekondari kuanzia julai mwaka 2009 kama ilivyoamuliwa na Serikali.

  Vyuo vya Ufundi

Kuna chuo kimoja cha ufundi. Maandalizi ya kujenga chuo kingine cha ufundi yameanza ili kukabiliana na changamoto za vijana wengi wanaomaliza shule na kukosa kuendelea na mafunzo ya sekondari .

Elimu ya Watu Wazima

Vipo Vituo 94 vya kisomo vyenye jumla ya wanafunzi 12,519 Kati ya hao 5312 ni wanaume na 6207 ni wanawake. Elimu ya Watu Wazima inakabiliwa na tatizo la mahudhurio duni, viwango vidogo vya malipo ya Walimu wa Kisomo, upungufu wa vifaa na vitendea kazi. Vile vile Vituo 42 vya MEMKWA vimeanzishwa vikiwa na wanafunzi 1005 sawa na wavulana 540 na wasichana 465

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
     
     
 
 
 
     
Copyright © 2008 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera, BUKOBA, TEL: 028 - 2220215/17, FAX: 027-2752184