JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - OFISI YA MKUU WA MKOA KAGERA
     
 
     
MISENYI
 
 
 
WILAYA YA MISENYI
 
[ Nyumbani ] au
 
   
HALMASHAURI YA WILAYA YA MISENYI
 
UTAWALA UTUMISHI         ELIMU MAFUNZO YA UFUNDI        
KILIMO MIFUGO USHIRIKA UJENZI ARDHI USTAWI WA JAMII MIPANGO URATIBU
BARABARA AFYA MAJI     MICHEZO MAENDELEO YA JAMII MAZINGIRA
...............................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................

UTANGULIZI

 

Halmashauri ya Wilaya ya Missenyi ni moja kati ya Halmashauri nane za wilaya za Mkoa wa Kagera. Halmashauri hii ilianzishwa tarehe 1, Julai, 2007 baada ya Halmashauri ya wilaya ya Bukoba kugawanywa katika halmashauri mbili (Halmashauri ya wilaya ya Missenyi na Halmashauri ya wilaya ya Bukoba)

 
 

MAHALI ILIPO KIJIOGRAFIA

 

Halmashauri ya Wilaya ya Missenyi ipo upande wa Kaskazini Mashariki ya Mkoa wa Kagera. Wilaya hii ipo kati ya Latitudo 1 o na 3 o Kusini ya mstari wa Ikweta na kati ya Longitudo 30 o 45' na 31 o 19' Mashariki ya Mstari wa Greenwich . Ipo mita 1,100 juu ya usawa wa Bahari. Hali hii inafanya Wilaya kuwa na misimu miwili ya mvua yaani vuli ambayo huanza Septemba na kumalizika Desemba na masika ambayo huanza Machi na kumalizika Juni. Kipindi cha Julai hadi mwanzoni mwa Septemba ni kiangazi. Kipupwe huanza Januari hadi Februari. Wilaya hii inapakana kwa upande wa Mashariki na ziwa Victoria na upande wa Kusini Wilaya ya Bukoba, Magharibi ni Wilaya ya Karagwe na Kaskazini ni Nchi ya Uganda . Wastani wa mvua kwa mwaka ni milimita 800 na 1,500 ambazo hufanya mimea kuwa na umbijani kwa mwaka mzima. Ipo mito mikubwa miwili ya Kagera na Ngono, Wilaya inayo ardhi ya vilima na mabonde yenye mito na matingatinga hasa kuelekea mto Kagera.

 

  ENEO

Halmashauri ya Wilaya ya Missenyi ina ukubwa wa kilometa za mraba 2,708.75 Eneo linalofaa kwa kilimo ni Ha. 99,726 na zinazolimwa ni Ha. 58,840 sawa na asilimia 59 ya eneo linalofaa kwa kilimo. Lipo eneo linalofaa kwa ufugaji hususani katika tarafa ya Missenyi ambapo kuna ranchi za taifa za Missenyi na Mabale. Sehemu ya ranchi hizi imebinafsishwa kwa wawekezaji.

IDADI YA WATU

Kulingana na sensa ya watu na makazi ya mwaka 2002, Halmashauri ya Wilaya ya Missenyi ina watu wapatao 152,842 , hadi kufikia Desemba, 2008 Halmasauri ya Wilaya Missenyi inakadiliwa kuwa na idadi ya watu 163,210. Msongamano wa watu ni 65 kwa kila kilometa moja ya mraba ya nchi kavu. Aidha ongezeko la watu ni asilimia 1.1. kwa mwaka.

Tarafa

Kiziba

Missenye

Jumla

Sensa ya 2002

61,863

90,979

152,842

Projection, 2008

66,059

97,151

163,210

Kaya

14,083

21,611

35,694

Wastani kwa Kaya

4.4

4.2

4.3

Asilimia ya ongezeko kwa mwaka

 

 

1.1

Eneo (Ha)

74,175

196,700

270,875

Idadi ya Watu kwa km 2

84

46

 

UTAWALA NA UWAKILISHI WA WANANCHI

Halmashauri ya Wilaya ina Tarafa 2, Kata 17, vijiji 74 na vitongoji 351. Kuna jimbo moja la uwakilishi Bungeni (Nkenge); Wilaya ina Madiwani 23 na Mbunge 1, kati ya madiwani hao 17 ni wa kuchaguliwa kutoka kwenye Kata na 5 ni kutokana na Viti Maalum.

MAENDELEO YA UCHUMI NA VITA DHIDI YA UMASKINI

Halmashauri ya Wilaya ya Missenyi ina Wadau (Stakeholders) mbalimbali wanaojishughulisha na shughuli za kusaidia kuleta maendeleo kwa wananchi ili kufanikisha juhudi za kuondoa umaskini. Wadau hao ni pamoja na Serikali Kuu, Vyama vya kuweka na kukopa, Wafanya biashara, Wavuvi na Asasi za kiraia na zisizo za Kiserikali na Programme za maendeleo kama vile TASAF.

KUONDOA KERO ZA WANANCHI NA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA

Kero na vitendo vya rushwa ni mambo yanayosababisha chombo au Serikali yeyote ichukiwe sababu ya kutokuwepo haki. Kama ilivyoainishwa katika Ilani ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2000. Wilaya imeendesha shughuli zake zikilenga kuondoa kero za wananchi na kupunguza au kuondoa kabisa mianya ya rushwa kwa njia zifuatazo:-

•  Taarifa za mapato na matumizi huwa wazi kwa umma.

•  Taratibu za ajira wakati wote zinazingatia miongozo na sheria.

•  Mipango ya maendeleo imeweka kipaumbele matakwa na inajibu hoja za wananchi mfano wake ni:-

•  Ujenzi wa madarasa.

•  Miradi ya kilimo na ufugaji.

•  Uimarishaji Vyama vya Ushirika ili viweze kutenda kazi kwa uwazi.

•  Mabaraza ya Kata yameundwa ili kusuluhisha migogoro miongoni mwa wananchi.

•  Halmashauri imeweka masanduku ya maoni ili kuwawezesha wananchi kutoa maoni yao na malalamiko yao na yanafanyiwa kazi kwa huandikwa kwenye rejista ya maoni ambayo hukaguliwa chini ya Mpango wa uboreshaji wa Serikali za Mitaa (yaani ni kigezo cha utawala bora)

•  Uendeshaji wa shughuli zote kwa njia za vikao:-

•  Baraza la Madiwani hutangazwa na huwa wazi kwa watu wote.

•  Mikutano Mikuu ya Mitaa/Vijiji hujadili kwa uwazi mambo yote yahusuyo maisha yao .

•  Vikao vya Mitaa/Vitongoji hutoa pia nafasi kwa wanavijiji kujadili kwa uwazi. Mambo yote yahusuyo maendeleo na maisha yao .

•  Vikao vingine kama vile Kamati za Kudumu za Madiwani, Wakuu wa idara, Serikali za Vijiji na Mikutano ya Mradi mbalimbali kama vile ya “World Vision (T)” na Partage hutoa nafasi za wahusika kwa niaba ya wale wanaowawakilisha.

 

UWEKEZAJI KATIKA SEKTA BINAFSI

Katika kuunga mkono juhudi za Serikali, Wilaya yetu imefungua milango kwa wawekezaji wa ndani na nje kuwekeza. Tumefanya jitihada kubwa kuboresha mazingira ya Wilaya yetu ili yavutie wawekezaji hao kuweka mitaji yao kwetu. Uboreshaji wa huduma za jamii zitolewazo Wilayani hapa kama kuwa na barabara nzuri zinazopitika muda wote, hali ya amani na utulivu, kuinua viwango vya uzalishaji wa mazao ya kilimo na biashara ni katika jumla ya mbinu za kuvutia wawekezaji katika Sekta Binafsi. Kutokana na hivyo, Wilaya imefanikiwa kupata wawekezaji katika maeneo mbalimbali kama ifuatavyo:-

  • Kiwanda cha Sukari Kagera (Kagera Sugar Limited) Sera ya Ubinafshaji imesaidia kufufuliwa kwa Kiwanda hiki ambacho kilisimamisha uzalishaji wake miaka saba (7) iliyopita. Mashamba ya miwa yenye ukubwa wa ekari 9500 yamelimwa na miundo mbinu ya Kiwanda imefufuliwa na kujengwa upya. Upanuzi wa mashamba bado unaendelea hadi lengo la ekari 20,000. Kiwanda kimeanza uzalishaji wa Sukari mwishoni mwa Oktoba, 2007. Hadi sasa Kiwanda kimetoa ajira kwa Watanzania katika fani mbalimbali wapatao 700 na pia hutoa ajira kwa wafanyakazi 1,300 kwa kazi za kutwa kila mwezi.
  • Katika kuitikia sera ya soko huria ili kuwapa mwanya wakulima kupata bei nzuri, wameruhusiwa wanunuzi mbalimbali wa kahawa kufanya hivyo. Wanunuzi hao ni Chama Kikuu cha Ushirika (KCU 1990 Ltd) na Kampuni Binafsi zaidi ya nne kwa Lengo ni kutoa bei nzuri kwa wakulima. Kwa sasa kampuni za ASU, LEGAL, KIPATO na AMRI HAMZA zinahusika na ununuzi wa kahawa Wilayani.

 

 

 

 

 

         
         
 
 
     
Copyright © 2008 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera, BUKOBA, TEL: 028 - 2220215/17, FAX: 027-2752184