JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - OFISI YA WAZIRI MKUU - TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA      
 
     
MISENYI
 
 
     
HALMASHAURI YA WILAYA YA MISSENYI
 
Halmashauri < [ Nyumbani ] au
 
 
BARABARA
 

Kuna jumla ya Km 724.9 za barabara. Kati ya hizo Km. 70.7 ni za Lami (Barabara kuu), Km 368 ni Changarawe na Km 286.2 ni za udongo. Barabara kuu ya lami imekuwa ni kiunganishi kizuri baina yetu na Nchi ya Uganda , na hivyo kuwa kichocheo kikubwa cha maendeleo ya Wilaya yetu.

 

 
 
 

SIMU

Kampuni za simu za mikononi za Zain, Tigo, Vodacom na Zantel zinatoa huduma ya simu za mikononi. Vilevile Kampuni ya simu ya Taifa TTCL nayo inatoa huduma za mawasiliano.

 
 

  POSTA

Kampuni ya Posta inaendelea kutoa huduma za usafirishaji wa barua na vifurushi.

Huduma za kifedha/benki

Kuna benki 1 ya “National Micro Finance Bank” (NMB) ambayo inatoa huduma ya kibenki hapa Wilayani. Huduma zinazotolewa ni pamoja na amana kwa wateja, mikopo kwa wajasiriamali na wafanya biashara wengine.

 

 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 

 

 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 
Hii ni moja ya barabara iliyotengenezwa kwa kiwango cha changarawe Wilayani Missenyi katika kijiji cha Byeju karibu na Mtukula.
 
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
     
     
 
     
Copyright © 2008 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera, BUKOBA, TEL: 028 - 2220215/17,