Halmashauri ya wilaya ya Missenye haina kumbi za burudani bali kuna ukumbi mmoja tu unaoendelea kujengwa huko kyaka katika wilaya hii kuna vilabu vya michezo 10 vinavyokamilisha usajiri na vilabu 3 ndivyo vimekamilisha na kusajiliwa kikiwemo cha Kagera sugar timu inayocheza ligi kuu
Kwaupande wa sanaa wilaya ina vikundi vya sanaa 3 ambavyo ni Missenyi ADP, Minziro na Ruzinga ambavyo vinajiendesha bila kuwa vimesajiri na BASATA, hivyo jitihada zinaendelea ili viweze kukamilisha taratibu za usajiri, aidha kamati ya michezo ya muda imeundwa ili kusukuma michezo na kuratibu usajilri wa vilabu na vyama vya michezo.
|