JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - OFISI YA MKUU WA MKOA KAGERA
     
 
     
KARAGWE
 
 
     
HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE
 
Halmashauri < [ Nyumbani ] au
 
 
 

ELIMU

 

ELIMU YA MSINGI

 

Katika kipindi cha mwaka 2006/07 mkazo mkubwa katika elimu uliendelea kuwekwa katika uandikishaji wa watoto, ukarabati na ujenzi wa vyumba vya madarasa, vyoo na upatikanaji wa vifaa vya Shule ikiwa ni pamoja na madawati, vitabu na Vivunge vya Hisabati (Science Kits).

 

IDADI YA SHULE

 

 

Shule za Awali

Wilaya ina Shule za Awali 97 zikiwemo 82 za serikali na 15 za binafsi zenye wanafunzi1151 (wavulana 529 na wasichana 622).

Shule za Msingi

Wilaya ina Shule 212 zikiwemo 204 za Serikali na 8 za binafsi zenye jumla ya wanafunzi 105,229 wasichana 53,491 na wavulana 51,738.

Idadi ya Walimu

Kuna Walimu 1,814 sawa na 69% ya Walimu 2628 wanaohitajika hivyo kuna upungufu wa Walimu 814. Uwiano wa Walimu kwa wanafunzi ni 1:72 walimu 9 wamerejeshwa kazini na wilaya imepata walimu wanafunzi 65 (Wanaume 41 na wanawake 24).

Madawati

Kuna madawati 31,610 sawa na 63.6% ya madawati 49,676 yanayohitajika hivyo kuna upungufu wa madawati 18,066.

Vyumba vya madarasa

Kuna vyumba vya madarasa 1,405 sawa na 55% ya vyumba 2,551 vinavyohitajika.

Nyumba za Walimu

Kuna nyumba za Walimu 343 sawa na 13.3% ya nyumba 2,576 zinazohitajika hivyo kuna upungufu wa nyumba 2,233.

Uandikishaji wa watoto

Uandikishaji wanafunzi ulifikia wanafunzi 19,744 (mwaka 2006. Aidha uandikishaji wa mwaka 2007 umefikia wanafunzi 15,915 ukilinganishwa na lengo la kuandikisha wanafunzi 16,283 sawa 98% ya lengo.

Ofisi

Kuna ofisi 293 sawa na 64% ya 458 ya ofisi zinazohitajika.

Stoo

Kuna stoo 88 sawa na 27.3% ya stoo 322 zinazohitajika kuna upungufu wa stoo 234. Juhudi za kuondoa upungufu uliotajwa hapo juu unaendelea kufanywa kwa kushirikisha wananchi na MMEM.

ELIMU YA SEKONDARI

Wilaya inazo sekondari 43 (zikiwemo 34 za serikali na 9 za binafsi). Sekondari zote zinaendelea kujengwa na juhudi zinafanyika kuhakikisha vyumba vya madarasa, Nyumba za Walimu na Majengo ya Utawala yanakamilika kukidhi mahitaji na Shule nyingine za sekondari zinaanzishwa ili kukidhi ongezeko la watoto wanaomaliza darasa la saba. Lengo lilikuwa ni angalau Sekondari moja katika kila Kata.

 

 

 


 
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 

 

 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 
 
 

AJIRA YA WALIMU

 

Katika mwaka 2006/07 wilaya ilipata walimu wapya 65, walimu waliopatikana pia ni wale waliokuwa wameacha kazi nao ni 9. Jitihada zinafanywa kuziba upungufu uliopo wa walimu. Kutokana na Walimu watakaopata ajira ya moja kwa moja kutoka vyuoni.

MMEM

Katika kipindi cha mwaka 2006/07 mkazo katika mpango wa maendeleo ya Elimu ya Msingi umewekwa katika, uanzishwaji wa madarasa ya Elimu ya Awali, uandikishaji wanafunzi darasa 1, ujenzi wa vyumba vya madarasa, ujenzi wa nyumba za Walimu, mafunzo kwa Kamati za Shule na ununuzi wa vitabu vya kiada. Aidha katika kipindi hicho jumla ya Tshs 682,474,041.= zililetwa kutoka hazina kwa ajili ya mpango wa MMEM kwa Mchanganuo ufuatao; Ujenzi wa madarasa Tsh.62,000,000.=. ujenzi wa Nyumba za Walimu Tshs 126.000.000.= Ununuzi wa Vitabu Tsh 197,777,308.80 Ununuzi wa vivunge vya Hisabati TShs.32,079,600.= na Utekelezaji halisi umekuwa kama ifuatavyo:-

•  Ujenzi wa madarasa 62,000,000.= kwa madarasa 20.

•  Ujenzi wa nyumba za Walimu 126,000,000.= kwa nyumba 35.

•  Ukarabati/mitihani/utawala 351,085,319.20.

•  Ununuzi wa vitabu 197,777,308.80.=

 

Kwa kuunga mkono juhudi za Serikali, wananchi wamechangia jumla ya TShs230,132,500.= katika ukusanyaji wa mawe, mchanga, kokoto, utengenezaji wa matofali, madawati na nguvu kazi.

Elimu ya Watu Wazima

Vipo vituo vya Ufundi Stadi 3 Isingiro (1), Nyaishozi (1) na Kibondo (1) vyenye jumla ya wanafunzi 70, wavulana 46 na wasichana 24. Pia zipo maktaba 107 kati ya mahitaji ya 204 na upungufu 97.

ELIMU YA UFUNDI

Wilaya inavyo vyuo viwili vilivyo rasmi vyenye matawi matatu (kikiwemo chuo kimoja cha Halmashauri ya Wilaya na chuo kimoja cha binafsi) vyuo hivi hutoa mafunzo ya Uashi, Useremala, Ufundi wa magari, Ufundi umeme, Udereva ushonaji na kuchomelea vyuma katika ngazi mbalimbali. Vyuo hivi huandikisha wastani wa wanafunzi 100 kila mwaka. Wanafunzi wa vyuo hivi wanafanya mitihani ya Taifa inayosimamiwa na VETA katika madaraja mbalimbali.

 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
     
     
 
 
 
     
Copyright © 2008 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera, BUKOBA, TEL: 028 - 2220215/17, FAX: 027-2752184