JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - OFISI YA MKUU WA MKOA KAGERA
     
 
     
KARAGWE
 
 
     
HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE
 
Halmashauri < [ Nyumbani ] au
 
 
 

MAENDELEO YA JAMII

 

 

Chini ya sekta hii juhudi zilizofanyika ni pamoja na kujenga uwezo wa jamii katika kutambua na kuandaa mikakati ya kutatua matatizo yake yenyewe. Aidha Halmashauri ikishirikiana na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto katika kipindi cha kuanzia 1998 jumla ya vikundi vya Wanawake 82 na Wanawake binafsi 65 vilipatiwa mikopo yenye thamani ya Tshs 43,002,500.= na zikirejeshwa na Riba Tshs 3,447,500.= Hadi kufikia 31/08/2007 kiasi cha shs. 36,089,612.= sawa na asilimia 77.6 ya fedha zimerejeshwa. Juhudi zinaendelea za kurejesha fedha zilizosalia kiasi cha Tshs 11,229,388.=. Wilaya pia inaendelea kufanya ufuatiliaji wa urejeshaji kwa kushirikisha kamati za mikopo za kata, Watendaji wa kata na vijiji ambapo wadaiwa wapo. Kwa kutumia fedha zilizokusanywa Shs. 22,000,000/=,SACCOS 4 zimekopeshwa ikiwa ni mikopo kwa vikundi vya akina mama.

 

 
 
 
ULINZI NA USALAMA

Juhudi za kuhakikisha hali ya usalama kwa wananchi na mali zao ziliendelea kufanyika japo kumekuwepo kupanda na kushuka kwa matukio ya wizi/unyang'anyi, mauaji na wizi wa mifugo. Wananchi na vyombo vya dola wanaendelea kushirikiana katika kuhakikisha hali ya usalama Wilayani inatengamaa. Aidha mwaka 2006/07 Serikali ilifanya operesheni maalum ya kuwarejesha watu wasio raia makwao na hadi sasa wahamiaji haramu wanaendelea kushughulikiwa kwa kutumia sheria za uhamiaji.

 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 

 

 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 
 
 
UTAWALA BORA NA DEMOKRASIA
 

Wananchi wameendelea kupata nafasi ya kushiriki katika maeneo mbalimbali ya siasa bila kubughudhiwa ikiwa ni pamoja na kutoa michango yao ya mawazo. Aidha wananchi wote wameelimishwa juu ya KERO YA RUSHWA na kutakiwa kuwataja wala rushwa katika maeneo yao . Hatua za kujaza nafasi za uwakilishi zinachukuliwa mara kwa mara. Mafunzo ya utawala bora kwa viongozi katika ngazi zote yalitolewa na yanaendelea kutolewa kwa kushirikiana na mpango wa maboresho ya serikali za mitaa (Local Government Reform Programme). Wilaya inaendelea na mpango wa maboresho ambapo pamoja na mambo mengine Wilaya inaweka hesabu zake kwa njia ya kompyuta kwa kutumia programu ya Epicor 7.8.

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
     
     
 
 
 
     
Copyright © 2008 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera, BUKOBA, TEL: 028 - 2220215/17, FAX: 027-2752184