Wilaya inao ng'ombe (kufikia Juni 2007) wa maziwa wapatao 5,575, ng'ombe wa asili 138,671, na ng'ombe walio ndani ya ranchi za Kikurula, Kitengule Magereza ni 20,150, mbuzi asili 133,407 wa maziwa 938, kondoo 13,220, kuku 73,484, nguruwe 1,256, Punda 10. Kutokana na ongezeko la ng'ombe wa kisasa na wa kienyeji uzalishaji wa maziwa uliongezeka toka lita 25,000,000 mwaka 2005 hadi lita 30,022,000 mwaka 2007. Tatizo kubwa linalowakabili wafugaji ni migogoro ya ardhi, magonjwa na wizi wa mifugo. Suala la migogoro ya ardhi linaendelea kushughulikiwa kupitia Mpango shirikishi wa matumzi bora ya ardhi.
Uzalishaji wa nyama Kg. 631,838.5 (2004/05), ngozi za ng'ombe vipande 5,255, ngozi za mbuzi vipande 3,478. Uzalishaji wa samadi kwa ajili ya kuzalisha Ndizi na Kahawa tani 561,700.
|