JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - OFISI YA MKUU WA MKOA KAGERA
     
 
     
KARAGWE
 
 
     
HALMASHAURI YA WILAYA YA KARAGWE
 
Halmashauri < [ Nyumbani ] au
 
 
 

UMEME

 

Wilaya inayo maeneo yenye vivutio vikubwa vya uwekezaji kibiashara, maeneo hayo yakipata umeme yatavutia sana wawekezaji, maeneo hayo ni:-

Maporomoko ya Murongo ( Murongo Falls )

Eneo hili kwa mujibu wa tafiti kadhaa ambazo zilishafanyika likiwekezwa na kuhudumiwa ipasavyo, lina uwezo wa kuzalisha umeme unaoweza kutosheleza maeneo ya Wilaya ya Karagwe, Ngara, Biharamulo na Wilaya za Bukoba na Misenyi. Kupatikana kwa umeme huo utaleta nafuu ya maisha, kuongeza biashara, kuongeza kipato na hatimaye kupunguza umasikini

 

 
 
 

Machimbo ya Bati Kyerwa

Eneo hili lina madini ya Bati mengi, kwa hiyo likiwekewa umeme, jamii itachimba na kuuza Bati hiyo na kusaidia kuongeza kipato kitakachosaidia kuondoa umaskini.

Maeneo ya mbuga za wanyama, mifugo na maeneo yenye historia

Maeneo ya mbuga: Ibanda na Rumanyika.

Maeneo ya Ranch: Zilizokuwa Ranch za Kitengule na Kikurura.

Eneo la kihistoria: Maeneo ya Bweranyange na Mtagata eneo lenye maji

yenye kutiririka yenye uvuguvugu na mandhari ya kupendeza.

 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 

 

 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 
 

Maeneo ya uzalishaji viwandani

Mji wa Kayanga na Omurushaka ni kati ya miji inayokuwa pia ni miji ya kibiashara na mwingiliano mkubwa wa shughuli za kiuchumi na kijamii, maeneo haya yanaendelea kuwekeza katika viwanda vya biashara kama viwanda vya kukoboa Kahawa, viwanda vya maziwa, kwa hiyo shughuli za uzalishaji zitaimarika pindi viwanda hivi vikipata umeme wa kutosha na wa kuaminika hivyo kuongeza uzalishaji, kupanua ajira, kukuza biashara ya uuzaji na ununuzi mazao tarajiwa hivyo kuongeza kipato na kukuza uchumi, hivyo kuboresha maisha ya jamii, kupunguza umaskini wa kipato na hivyo kuchochea kasi ya kuondoa umaskini.

Vile vile, Dira hii, inalenga kuimarisha miji midogo inayokua ya Isingiro, Murongo, Nkwenda, Nyaishozi, Kamuli, Mabira, Nyabiyonza, Bugomora na Ihembe (kwa kuanzia). Miji hii inayokua kibiashara, ikipata umeme itaongeza uzalishaji hivyo kukuza kipato, kuongeza ajira, kuongeza uzalishaji wa bidhaa hali itakayosaidia kupunguza umaskini.

 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
     
     
 
 
 
     
Copyright © 2008 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera, BUKOBA, TEL: 028 - 2220215/17, FAX: 027-2752184