JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - OFISI YA MKUU WA MKOA WA KAGERA
     
 
     
CHATO
 
 
     
HALMASHAURI YA WILAYA YA CHATO
 
Halmashauri < [ Nyumbani ] au
 
 

SEKTA YA AFYA

 

Sekta hii imeendelea kutekeleza sera ya afya (Tiba na Kinga).

 
 
 
 

Huduma za Tiba

 

Wilaya ina jumla ya vituo 20 vinavyotoa h uduma za tiba na kinga kama inavyoonyeshwa katika mchanganuo ufuatao:

Aina

Serikali

Binafsi

Jumla

Hospitali

1

-

1

Vituo vya Afya

1

-

1

Zahanati

16

2

18

JUMLA

18

2

20

 
 
 
Elimu ya Afya
 

Elimu ya Afya imeendelea kutolewa katika Vituo vyetu vya huduma za Afya wagonjwa katika Hospitali, vituo vya Afya, Zahanati, na katika kliniki za akina mama wajawazito na watoto. Elimu dhidi ya UKIMWI imepewa kipaumbele kwa kushirikisha jamii, ambapo viongozi wa ngazi mbali mbali wakiwemo viongozi wa madhehebu ya dini na siasa wamesaidia kuelimisha jamii kuhusu janga hatari la UKIMWI.

 
Mahudhurio ya Kliniki na Chanjo kwa Mwaka 2007
 

Wajawazito 13,977 walitarajiwa walihudhuria kliniki mwaka 2007, waliohudhuria ni 13,949 (99.8%). Kati ya waliohudhuria, wajawazito 12,833 (92%) walipata chanjo ya pepopunda. Miongoni mwa watoto 13,977 walio chini ya umri wa mwaka mmoja waliotarajiwa kupata chanjo, watoto 13,432 (96.1%) walikamilisha chanjo zote zilizotakiwa.

 

 

Vifo vya Akina Mama Wajawazito

Katika mwaka 2007 kulitokea vifo vya mama wajawazito 12 kati ya watoto hai 21,782 waliozaliwa. Hii ni sawa na akina mama 55 kwa kila watoto hai 100,000 waliozaliwa.

 
Jitihada za kupambanana na matatizo ya kiafya Wilayani
 

•  Elimu ya afya imeendelea kutolewa katika vituo vyote vya matibabu wilayani.

•  Chunguzi za kina zinafanyika kwa vifo vya akina mama vinavyotokana na uzazi ili kubaini vyanzo na kutafuta ufumbuzi.

•  Matumizi ya vyandarua vyenye dawa yameendelea kuhimizwa ili kupunguza mambukizi ya malaria, hii ni pamoja na mpango wa usambazaji wa vyandarua kwa hati punguzo unaoendelea kwa akina mama wajawazito.

•  Elimu dhidi ya ugonjwa wa UKIMWI inaendelea kutolewa, vituo vya upimaji wa VVU vimeongezwa, na wale wote wenye kuhitaji huduma ya dawa za kurefushamaisha (ART) wanapata huduma hiyo katika hospitali ya wilaya.

 

Ujenzi wa Vituo vya Afya na Zahanati Katika Kila Kijiji na Kata

 

Zoezi la uhamasishaji limeanza katika kata na vijiji vyote wilayani Chato kwa kushirikisha viongozi wa ngazi zote na wananchi. Vijiji viwili vimeanza ujenzi wa zahanati (Kibumba na Nyambiti) na kata moja (Kachwamba) imeanza ujenzi wa kituo cha afya. Zahanati zote na kituo cha afya vinaendelea kukarabatiwa kwa nguvu za wananchi na fedha kutoka serikalini (General rehabilitation fund - GRF).

Kila kijiji kimetakiwa kutenga eneo kwa ajili ya ujenzi wa zahanati na kila kata kutenga eneo kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya. Katika maandalizi haya, kila kijiji kinatakiwa kuchangia matofali 500,000 ya kuchoma, na pia kukusanya mawe na mchanga.

CHANGAMOTO KATIKA SEKTA YA AFYA WILAYANI

  • Upungufu mkubwa wa watumishi (Madaktari na Wauguzi).
  • Upungufu wa majengo ya wodi za kulaza wagonjwa katika hospitali ya wilaya, vituo vya afya na
  • Upungufu wa vitendea kazi (x-ray, ultra sound, na magari)

 

 

 
 
 
 
 
MAPAMBANO DHIDI YA JANGA LA UKIMWI
 

Wilaya inaendeleakutoa elimu kwa wananchi kuhusu ugonjwa wa UKIMWI kupitia vituo vya tiba, vikundi vya burudani, maeneo ya ibada na mikutano ya hadhara.

Wilaya imeanzisha programu ya kuzuia maambukizo ya virusi ya UKIMWI kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto (PMTCT). Kwa kipindi cha mwaka 2007 jumla ya akinamama wajawazito 2,043 walipima VVU na kati ya hawa 55 (2.7%) waligundulika na maambukizi ya VVU. Hadi Desemba 2007 wilaya imeanzisha jumla ya vituo 9 vya kuzuia maambukizo toka kwa mama kwenda kwa mtoto (PMTCT).

Wilaya ina vituo 5 vinavyotoa huduma ya ushauri nasaha na upimaji wa virusi vya UKIMWI kwa hiari (VCT). Kwa kipindi cha Januari hadi Juni, 2007 jumla ya watu 1,761 walijitokeza kupima virusi vya UKIMWI kwa hiari, kati ya hawa waliogundulika na maambukizi ya virusi vya UKIMWI walikuwa 134 (7.6%).

Wilaya ina kituo kimoja kinachotoa dawa za kurefusha maisha. Katika kipindi cha januari hadi Desemba, 2007 wilaya iliweza kutoa dawa za kurefusha maisha kwa jumla ya wagonjwa 211 kati ya watu 542 waliosajiliwa.

 

 

Mipango ya Baadae ya Zoezi la Upimaji na Udhibiti wa Kusambaa kwa Ukimwi na Kusaidia Walioathirika

 

Baada ya kampeni, zoezi la upimaji wa VVU linaendelea kutolewa katika vituo vitano (5) katika sehemu mbalimbali wilayani Chato. Vile vile huduma ya kuzuia maambukizo ya mama kwenda kwa mtoto inaendelea kutolewa katika vituo viwili (2).

Huduma ya matibabu kwa walioambukizwa VVU pia inatolewa katika Hospitali ya wilaya ya Chato (kituo cha huduma tiba na matunzo CTC). Hadi kufikia 14/12/2007 jumla ya wagonjwa 536 wameandikishwa na wanaendelea kupata matibabu.

 
Mikakati ya Wilaya Kukabiliana na Janga la Ukimwi Mwaka 2008

•  Kuongeza idadi ya vituo vinavyotoa huduma za ushauri Nasaha na upimaji wa VVU kwa hiari toka vituo 4 vilivyopo sasa hadi vituo 10.

•  Kuongeza idadi ya vituo vinavyotoa huduma za kuzuia maambukizo ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto (PMTCT) toka vituo 2 vilivyopo sasa hadi 10.

•  Uimarisha kituo cha huduma, Tiba na matunzo kwa watu wanaoishi na VVU (CTC) kilichopo Hospitali ya Chato kukifanyia ukarabati na kuongeza vifaa vya kupimia kama CD4 Count machine n.k.

•  Kupanua huduma za Tiba na matunzo (CTC) kwa kuanzisha vituo vingine vipya vine (4), ambavyo ni kituo cha Afya Bwanga, Zahanati za Katete, Kasenga na Buseresere.

•  Kuimarisha huduma za wagonjwa nyumbani kwa kuboresha mfumo wa ufuatiliaji na rufaa kwa kushirikisha vikundi mbalimbali vya kijamii (CBOs, NGOs na FBOs).

•  Kutambua na kuimarisha vikundi vya sanaa na maonyesho vinavyohamasisha mapambano dhidi ya UKIMWI.

•  Kuimarisha kamati za kudhibiti UKIMWI ngazi ya kata vijiji na vitongoji.

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
     
     
 
 
 
     
Copyright © 2008 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera, BUKOBA, TEL: 028 - 2220215/17, FAX: 0282752184