JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - OFISI YA MKUU WA MKOA KAGERA
     
 
     
CHATO
 
 
     
HALMASHAURI YA WILAYA YA CHATO
 
Halmashauri < [ Nyumbani ] au
 
 
 
 

SEKTA YA KILIMO (MAZAO)

Uzalishaji wa Mazao msimu uliopita wa 2006/07 na mavuno

Utekelezaji wa malengo ya Kilimo kwa msimu wa 2006/07 kwa Wilaya ya Chato ni kama inavyooneshwa hapa chini

Mazao ya Chakula

Na.

Zao

Lengo (Ha.)

Matarajio ya Mavuno (MT)

Utekelezaji (Ha.)

Mavuno Halisi (MT)

1.

Mahindi

23,346

29,265

22,916

34,082

2.

Maharage

7,499

3,235

7,124

3,749

3.

Mtama (chakula)

3,969

5,556

709

993

4.

Muhogo

27,874

139,400

28,226

225,808

5.

Viazi vitamu

10,859

43,412

7,958

31,832

6.

Mpunga

2,000

3,778

1,760

5,280

7.

Karanga

2,967

2,047

2,087

1,460

8.

Ulezi

622

313

427

214

9.

Uwele

287

255

216

130

 

Jumla

79,423

227261

71,423

303,548

Kutokana na takwimu ya idadi ya watu Wilayani Chato kwa mwaka 2007, mahitaji halisi ya chakula ni MT 95,472 ya nafaka kavu (baada ya kutoa maji maji). Kutokana na mavuno ya msimu wa 2006/2007 MT. 303,548 ya nafaka na mihogo, Wilaya ina ziada ya MT. 208,076

Mazao ya Biashara

Na.

Zao

Lengo (Ha.)

Matarajio ya Mavuno (MT)

Utekelezaji (Ha.)

Mavuno (MT)

1.

Pamba

14,052

12646.8

8,072

3,238

Hali ya Mvua Kwa Msimu wa 2007/08

Katika msimu wa kilimo 2007/2008, mvua zilianza kunyesha mapema sana, Mvua zimeanza kunyesha katikati ya mwezi wa Agosti kama jedwali linavyoonyesha hapa chini:

Mwezi

Kiasi (mm)

Idadi ya siku

Agosti

85.9

4

Septemba

80.3

2

Oktoba

60

3

Novemba

164.1

14

Hadi Desemba,31

113.2

9

Jumla

503.5

32

Pamoja na mvua kuanza mapema, zimeendelea kunyesha katika mtiririko/mtawanyiko mzuri kiasi cha kufanya mazao yaliyoko mashambani kuwa katika hali ya kuridhisha. Kwa mazao yaliyopandwa katikati ya Oktoba halikadhalika yanaendelea kukua vizuri

Ununuzi wa Mazao ya Biashara Msimu 2006/07

(i) Pamba:

Msimu wa ununuzi wa pamba ulifunguliwa tarehe 25/6/2007 . Jumla ya kampuni 6 za Kahama oil Mills, Kahama Cotton Company, Mass Trading Company, Cop - Cot Company, Birchand na Dimond Ginning Company zilipewa kibali cha kununua pamba mbegu Wilayani. Hadi Novemba, 2007 jumla ya Kg 3,238,047 zimenunuliwa. Bei ya kuuzia kwa kilo ilikuwa kati ya Tshs. 325/= hadi Tshs. 550/=. Bei hizi ni kwa wastani wa Tshs. 437.50 kwa kilo. Wananchi walijipatia jumla ya Tshs. 1,416,645,563/=.

Hali ya Pembejeo kwa Msimu 2006/07

Upatikanaji wa mbegu bora za Mahindi na mtama zimekuwa zikipatikana kwa wafanya biashara binafsi. Wafanya biashara wa pembejeo hizi wanapatikana katika Kata za Buziku, Bwanga, Chato, Buseresere na Muganza.

Aidha, Wilaya ilipata mbolea ya ruzuku aina ya UREA Tani 5 na zilisambazwa kwa walengwa na ilitumika sana katika maeneo yanayolima kilimo cha bustani kandokando mwa ziwa Victoria.

Upatikanaji wa Pembejeo kwa Msimu wa 2007/08

Wilaya ya Chato na Mkoa wa Kagera kwa ujumla haimo katika orodha ya Wilaya zitakazostahili kupata mbolea ya ruzuku. Hii ni kufuatia maelezo ya Wizara kupeleka mbolea katika mikoa maalumu inayolima nafaka kwa wingi. Hata hivyo yako maduka ya pembejeo za kilimo katika miji ya Chato,Buziku,Buseresere na Muganza.

Matumizi ya mbolea bado yako chini, hata hivyo wakulima wanaendelea kupewa elimu juu ya matumizi ya mbolea za viwandani, samadi na mboji kupitia mashamba darasa. Wilaya pia imepokea viuwadudu vya zao la pamba kiasi cha chupa 25,600 zenye ujazo wa 200ml toka Bodi ya Pamba na usambazaji kwa wakulima unaendelea wilayani kote.

Hali ya Kilimo cha Wanyamakazi

Wilaya ya Chato kwa sehemu kubwa inafaa kuendesha shughuli za kilimo kwa kutumia zana mbalimbali zinazokokotwa na wanyamakazi. Aidha kumekuwepo na ongezeko la matumizi ya wanyamakazi katika shughuli za kilimo.

Aidha katika msimu wa kilimo wa 2006/2007, jumla ya kaya 2,387 kati ya 47,736 sawa na asilimia 5% zinatumia wanyamakazi katika shughuli za kilimo.

Katika Msimu wa Kilimo wa 2007/08 Wilaya imepokea zana mbalimbali zinazokokotwa na wanyamakazi toka Ofisi ya Kanda Umwagiliaji kama ifuatavyo:Ox-Plough 8,Magoye rippers 8,Cultivators/weeders 8,Jab Planters 2,Direct Seeder1na chains 8 na zana hizi zimesambazwa katika vikundi vya wakulima vilivyopatiwa mafunzo na baadhi ya zana hizi zitarudishwa katika kituo cha mafunzo Buziku (OTC) kikishakamilika.


 
 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 

 

 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 
 
 
 
 

Mkakati wa Wilaya Kuongeza Uzalishaji wa Kilimo

Wilaya imejipanga kuongeza uzalishaji wa mazao ya kilimo na Mifugo kama ifuatavyo:-

•  Pamba : Kuongeza uzalishaji kwa ekari toka Kilo 260 hadi 1,000.

•  Mahindi : Kuongeza uzalishaji toka kilo 300 kwa ekari hadi Kilo 1,350

•  Muhogo : Kuongeza uzalishaji toka kilo 760 za mhogo mkavu kwa ekari hadi Kilo 1,000

•  Mpunga : Kuongeza uzalishaji toka kilo 1,200 za mpunga kwa ekari hadi Kilo 2,400

•  Mtama : Kuongeza uzalishaji toka kilo 300 kwa ekari hadi Kilo 1,000

Ili kufikia malengo yaliyotajwa hapo juu, Wilaya imejipanga kufanya yafuatayo:-

•  Kuongeza matumizi ya mbolea za asili na viwandani kwa mazao yote ya Chakula na Biashara.

•  Kuimarisha usimamizi, uratibu na tathmini ya shughuli kuanzia ngazi ya kitongoji hadi ngazi ya Wilaya.

•  Kuimarisha huduma za ugani kwa mazao ya chakula na biashara.

•  Kuimarisha kilimo cha umwagiliaji kwa kuendelea kuunda vikundi, kuvipa mafunzo na kuvipatia mashine za umwagiliaji.

•  Kuimarisha na kusimamia kilimo cha Wanyamakazi

Utekelezaji wa Mkakati hadi sasa.

  • Wilaya imeandaa rejesta za kuratibu huduma za ugani kwa wataalamu wa ugani ambazo zimeshasambazwa hadi ngazi ya Vijiji,rejesta hizi zinamtaka bwana shamba asaini kwenye rejesta yake na iliyoko kijijini kila anapotoa huduma ya ugani na wale anaowahudumia wathibitishe na zinakaguliwa na ofisi ya kilimo na task force ya Wilaya kwa ujumla.
  • Tayari mashamba darasa 32 ya mazao mbalimbali yameanzishwa kupitia mradi wa uwekezaji katika sekta ya kilimo (DASIP) na yanaendelea vizuri ambayo ni kama ifuatavyo:19 mahindi,8 pamba,3 muhogo,1 mpunga,1 vitunguu.
  • Vikundi 42 vya umwagiliaji vimeshaundwa na kupewa mafunzo sambamba na kupewa mashine na zana mbalimbali za umwagiliaji.vikundi 19 vinaendelea kupata mafunzo ya umwagiliaji kupitia mradi wa FAO .
  • Wilaya kupitia walezi wake wa Kata inaendelea kufuatilia utekelezaji wa mkakati kwa karibu ngazi ya vijiji na vitongoji.
 
 

 

Kilimo cha Umwagiliaji Maji Mashambani

Maeneo ya Umwagiliaji

Wilaya ya Chato inayo maeneo yanayofaa kwa kilimo cha umwagiliaji. Maeneo hayo ni kama ifuatavyo:-

Na.

Eneo la Kilimo

Ukubwa wa eneo (Ha.)

1.

Katete

60

2.

Itale/Chato

400

3.

Masasi

1,000

4.

Nyakato

1,000

5.

Buzirayombo

150

6.

Bukome/Nyabilezi

300

7.

Nyamirembe

600

8.

Busaka

1,000

9.

Nyarwambu

3,000

10.

Rubambangwe

200

11.

Musasa

3,000

Jumla

10,710

Kwa sasa eneo linalotumika katika kilimo cha umwagiliaji limeweza kuongezeka toka hekta 40 hadi kufikia hekta 200 hii imetokana na mchango wa mashine za umwagiliaji zilizotolewa na shirika la Chakula Duniani FAO.

 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
     
     
 
     
Copyright © 2008 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa KAGERA, BUKOBA, TEL: 028 - 2222341/18, FAX: 028-2221356