JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - OFISI YA MKUU WA MKOA KAGERA
     
 
     
CHATO
 
 
     
HALMASHAURI YA WILAYA YA CHATO
 
Halmashauri < [ Nyumbani ] au
 
 
SEKTA YA MIFUGO
 

Hali ya Ulaji wa Nyama na Unywaji wa Maziwa

Mazao ya mifugo yanayopatikana ndani ya wilaya ni maziwa ya ng'ombe, Nyama ya ng'ombe na ile ya wanyama wadogo pamoja na ndege. Ng'ombe 5,011 mbuzi 4,665 na nguruwe 59 walichinjwa na kuzalisha nyama kilogramu 652,100 yenye thamani ya Tshs. 1,173,780,000 kwa mwaka 2007, ukilinganisha na kilogramu 400,860 yenye thamani ya Tshs. 601,290,000 kwa mwaka 2006. , Aidha inakadiliwa kuwa zaidi ya Lita 14,230,080 za maziwa zilizalishwa kwa mwaka 2007. Kutokana na takwimu hizo wastani wa unywaji wa maziwa kwa mtu mmoja ni lita 45 kwa mwaka.

 

 
 

Aina ya Mifugo na Idadi iliyopo Wilayani:

Na.

Aina ya Mifugo

Idadi

•   

Ng'ombe wa asili

72,569

•   

Ng'ombe wa maziwa

34

•   

Kondoo

8,234

•   

Nguruwe

153

•   

Kuku wa asili

84,522

•   

Kuku wa mayai

0

•   

Kuku wa nyama

0

•   

Bata

23,012

•   

Sungura

43

•   

Mbwa

2,574

•   

Punda

87

•   

Paka

56

•   

Kanga

42

 

Jumla

191,326

Hali ya Masoko ya Mifugo na Mazao yake

Wilaya ya Chato inayo Minada 2 ya mifugo iliyoko Bwanga na Buzirayombo. Katika kipindi cha mwaka 2006/2007, ng'ombe 5,164 wenye thamani ya Tshs. 1,032,800,000 wameuzwa kupitia minada hii. Nyama, maziwa na mayai ya kuku yamekuwa yakiuzwa moja kwa moja kwa walaji wa ndani ya Wilaya bila kusindikwa, kwa kiwango cha wastani wa Tshs 1,800/= kwa kilo ya nyama, Tshs 300/= lita ya maziwa na Tshs 150/= kwa yai moja.

 

 
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 

 

 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 
 
 
 
 

Mkakati wa Wilaya Kuboresha Ufugaji

Wilaya imejiwekea mikakati ifuatayo:-

•  Kuboresha upatikanaji wa malisho ya mifugo na maji

•  Kuwahimiza wafugaji kutekeleza kanuni za ufugaji bora na kuwawezesha kuingia kwenye ufugaji wa kisasa na kibiashara unaozingatia ubora zaidi kuliko wingi wa mifugo.

•  Kuboresha afya ya mifugo

•  Kuwezesha upatikanaji wa nyama safi na bora kwa walaji.

•  Kuhamasisha wawekezaji kuwekeza kwenye sekta ya mifugo

Utekelezaji wa mkakati hadi sasa

  • Wilaya kupitia mpango wa kilimo ijenga lambo 1 la kunyweshea mifugo
  • Wilaya inaendelea kuhamasisha wafugaji juu ya matumizi bora ya ardhi ikiwa ni pamoja na kutenga maeneo ya malisho na kuwahimiza kupunguza mifugo yao na tayari Wilaya imepitisha uanzishaji wa mnada wa mbuzi wa Katende.
  • Wilaya inajenga vibanio 4 kupitia mradi wa DASIP kwa ajili ya shughuli za chanjo, pia Maafisa ugani wameendelea kutoa mafunzo ya uongeshaji kwa kutumia kinyunyizio mbeleko na Majosho.
  • Machinjio 1 inaendelea kujengwa katika mji mdogo wa Buseresere.

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
     
     
 
     
Copyright © 2008 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa KAGERA, BUKOBA, TEL: 028 - 2222341/18, FAX: 028-2221356