JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - OFISI YA WAZIRI MKUU - TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA      
 
     
CHATO
BIHARAMULO
 
 
     
HALMASHAURI YA WILAYA YA CHATO
 
Halmashauri < [ Nyumbani ] au
 
 
SEKTA YA USHIRIKA
 

Maendeleo ya Vyama vya Akiba na Mikopo (SACCOS)

Wilaya ina vyama vya Ushirika kama ifuatavyo:-

SACCOS 19 zenye wanachama 3,086, AMCPS 28, Chama cha Wavuvi 1. Pia kuna vikundi vidogo vidogo 323 vya uzalishaji mali ambavyo vimejiunga na SACCOS. Aidha kuna Chama cha Ushirika 1 (BCU).

Hisa zilizokusanywa toka katika SACCOS ni Tshs. 29,586,000/=, akiba zilizokusanywa ni Tshs. 274,376,000/= na amana ni Tshs. 317,985,000/=. Jumla ya mtaji ni Tshs. 621,947,000/=. Mikopo iliyokopeshwa ni Tshs. 854,800,000/=. Mikopo iliyorejeshwa ni Tshs. 356,657,000/= na ambayo bado kurejeshwa ni Tshs. 498,143,000/= ambayo iko katika mzunguko.

Awamu ya Kwanza ya Utekelezaji wa Mpango wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi

Halmashauri ya Wilaya kupitia Afisa Ushirika na Madiwani katika maeneo yao iliwahamasisha wananchi kujiunga kwa wingi katika SACCOS zilizopo katika maeneo yao ili waweze kuboresha miradi yao binafsi kwa kuomba mikopo yenye riba nafuu katika awamu ya kwanza. Maombi 427 yenye thamani ya Sh. 1,512,099,000 yalipokelewa NMB Tawi la Biharamulo. Maombi matatu ya Mwambao SACCOS, Mshikamano SACCOS na Angaza SACCOS yenye thamani ya Tshs. 100,000,000 lilipokelewa na kukopewshwa.

Mpaka kufikia tarehe 31, Desemba 2007 Mwambao SACCOS imekwisha rejesha CRDB Tshs.41,000,000, fedha ambazo bado hazijarejeshwa zipo katika mizunguko.

 

 

 
 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 

 

 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 
 
 
 
 

Awamu ya Pili ya Mpango wa Uwezeshaji wa Wananchi Kiuchumi

•  Halmashauri kupitia Wataalam wa Ushirika imewahamasisha wanachama wa SACCOS katika mikutano mikuuu ya vyama ili waweze kujipanga mapema na kujielekeza vizuri namnaya kubuni miradi binafsi ya maendeleo kwa kila mwanachamaili waweze kukopa fedha hizo zenye masharti nafuu

•  Halmashauri kupitia wataalam wake imeweka mkakati wa makusudi kuendesha mafunzo zaidi jinsi ya kuandika maandiko ya Miradi ikiwa ni pamoja na uendeshaji wa shughuli zote za ujasiriamali.

•  Mafunzo ya Ujasiliamali yanaendelea kwenye Kata zote 14, hadi sasa Kata 9 zimeshapata mafunzo.

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
 

 

 
 
 
 
     
     
 
     
Copyright © 2008 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera,BUKOBA, TEL: 028 - 2222341/18, FAX: 028-2221356