Lengo kuu la sekta hii ni kuendeleza na kuimarisha mazingira ya upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi wa wilaya hii kwa kutumia teknolojia sahihi na rahisi inayokubalika na yenye gharama nafuu kiuendeshaji.
Wilaya ya Chato ina watu 318,240 kati yao wakazi 72,867 ambao ni 23% ya wakazi wote wanapata maji safi na salama kutokana na vyanzo kama inavyoonyeshwa katika jedwali hapo chini. Pia Inatarajiwa kuwa ifikapo mwaka 2010 idadi ya Wakazi 190,944 sawa na 60% ya wakazi wote Wilayani watapata maji safi na salama kupitia programu ya maji na usafi wa mazingira. |