Katika kukabiliana na uharibifu huo, Wilaya imeweka mikakati ifuatayo ambayo inaendelea kutekelezwa:
Kuwaondoa wavamizi wafugaji na mifugo kwenye maeneo waliyovamia: “Operation” ya kuondoa mifugo katika misitu ya hifadhi na mapori imefanyika.
Matumizi bora ya teknolojia ya nishati: Katika suala la kuhifadhi misitu, wilaya inaendeleza teknolojia ya matumizi bora ya nishati kwa kutengeneza majiko sanifu.
Kuwa na Mpango kamambe wa matumizi bora ya ardhi uwe umehuishwa na kusambazwa vijijini. Mafunzo juu ya matumizi bora ya ardhi yametolewa katika vijiji 74 na vijiji vyote vimeshatengeneza Mipango kamambe wa matumizi bora ya ardhi. Kazi iliyopo sasa ni kuihuisha mipango hiyo.
Kuwajibisha Uongozi wa eneo husika utakaoshindwa kutekeleza zoezi la kudhibiti matukio ya moto katika maeneo yao. Viongozi wa ngazi zote wameshaelekezwa juu ya suala hili.
Operesheni ya kukamata mkaa, kuni na mbao inaendelea kufanyika na wahusika kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.
|