HALI YA UPIMAJI WA HIARI WA VIRUSI VYA UKIMWI-KAMPENI YA KITAIFA ILIYOZINDULIWA RASMI KI-WILAYA TAREHE 22-9-2007
LENGO LA WILAYA KATIKA UPIMAJI
Lengo la Wilaya lilikwa ni kupima idadi ya watu 8,700, lakini kutokana na
kushirikisha jamii kwa kutoa elimu juu ya faida ya kupima kwa hiari, kushirikisha wadau mbali mbali kama vile mashirika yasiyokuwa ya Kiserikali, Mashirika ya kijamii, na Mashirika ya Dini kabla ya utekelezaji wa zoezi zima la upimaji limeleta mafanikio makubwa katika kufanikisha zoezi hilo .
Katika utekelezaji wa kampeni ya upimaji wa hiari, uhamasishaji wa jamii kwa njia ya sanaa, Mikutano ngazi ya jamii, kujituma kwa Watendaji na Viongozi mbali mbali, kumewezesha Wilaya kuvuka lengo la kupima watu 8,700, hivyo kupelekea Mkoa kutoa lengo la pili la idadi ya watu 15,000, ambapo Mpaka kufikia mwezi Desemba 2007 Jumla ya Watu waliojitokeza kupimwa imefikia 24,491 . Wilaya ilikuwa na idadi ya vituo 28 (VCT) vilivyotumika katika upimaji wa VIRUSI VYA UKIMWI)
|