MAJI
Lengo kuu la sekta hii ni kuendeleza na kuimarisha mazingira ya upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi wa wilaya hii kwa kutumia teknolojia sahihi na rahisi inayokubalika na yenye gharama nafuu kiuendeshaji.
Hadi sasa asilimia ya wakazi wa wilaya wanaopata maji safi ni 38.0
Ili kufikia azma hii, Wilaya ilijiwekea mikakati ifuatayo ili kufikia lengo la kuwapatia wananchi wake maji safi na salama kwa umbali ulio karibu: (Ndani ya mita 400)
Kuendeleza uchimbaji wa visima vifupi vya maji na kuimarisha vyanzo vya asili na utunzaji wake.
Kuendeleza teknolojia ya uvunaji wa maji ya mvua
Kujenga na kuendeleza miradi ya maji ya bubujiko.
Kushirikisha wananchi kikamilifu katika kuhudumia miradi ya maji na matumizi ya maji hayo – (kuwashirikisha tangu hatua ya kupanga hadi uendeshaji).
Kuimarisha vikundi vya watumiaji maji (WUGs).
Kutokana na vyanzo mbalimbali vya maji vilivyopo wilayani, jumla ya wakazi 80,228 ambao ni asilimia 38 ya wakazi wote wilayani wanapata maji kutokana na vyanzo kama inavyoonyeshwa katika jedwali hapo chini.Pia Inatarajiwa kuwa ifikapo mwaka 2010 idadi ya Wakazi 106,956 sawa na asilimia 54 ya wakazi wote Wilayani watapata maji safi na salama.
Upatikanaji wa maji katika mji wa Biharamulo
Mji wa Biharamulo una idadi ya wakazi 15,000. Kati ya hao Wakazi 10,000 wanapata maji ambayo ni sawa na asilimia 67. Upatikanaji wa maji katika Mji wa Biharamulo ni kwa njia zifuatazo, Maji ya bomba (ya kusumwa na mashine), Mradi wa mububujiko (Gravity), na Vyanzo vya asili vilivyoboreshwa. Inatarajiwa kuwa ifikapo mwaka 2010 idadi ya Wakazi 11,250 sawa na asilimia 75 watapata maji safi na salama.
Mikakati iliyowekwa kufikia lengo hili ni pamoja na Kukarabati vyanzo 3 vya maji na mataki 5 ya kuhifadhi maji.
Kufunga bomba mita 18,000 maeneo mapya ya Mji
Kununua mitambo 5 ya kusukumia Maji
-
Kujenga matenki 4 yenye ujazo wa m3 6000
Kukarabati mabomba ya kusambazia maji yenye urefu wa mita 20,0000
Kuhamasisha Wananchi umuhimu wa kutunza miundo mbinu ya maji na uhifadhi wa maji
|