Lengo kuu la sekta ya Maendeleo ya Jamii ni kuchukua hatua zinazowawezesha watu kutambua uwezo walio nao wa kubaini matatizo na uwezo wao wa kutumia raslimali zilizopo kujitatulia matatizo hayo, kujipatia na kujiongezea kipato na kujiletea maisha bora zaidi na hivyo kujiletea maendeleo, na kuweka mazingira muafaka yatakayo wawezesha wanawake na wanaume kutekeleza majukumu yao katika jamii kwa kuzingatia mahitaji ya kijinsia. Aidha lengo jingine ni kuongeza ushirikishwaji wa wanawake na vijana katika shughuli za maendeleo, hatimaye kuleta maisha bora kwa kila mtanzania.
Kazi zinazotekelezwa na sekta ya Maendeleo ya Jamii katika mkoa wa Kagera ni pamoja na:-
Kujenga uelewa wa wananchi ili aweze kushiriki shughuli mbalimbali za kujiletea maendeleo yao kwa njia ya kujitegemea na kuwasaidia kupanga mipango inayotekelezeka.
Kuhamasisha wananchi kujiunga katika vikundi vya kijamii na SACCOS ili kuanzisha na kutekeleza shughuli za uzalishaji mali zenye kuchangia kuinua hali zao za maisha, pamoja na utoaji wa mikopo ya kiuchmi kwa wananwake kupitia mfuko wa maendeleo ya jamii wa wanawake.
Kushirikisha jamii katika mapambano dhidi ya janga la UKIMWI na kutoa msaada kwa watoto yatima.
Kusaidia jamii jinsi ya kuondokana na mila potofu zinazochangia kuzorotesha maendeleo ya wananchi.
TATIZO LA UKIMWI:
Kama inavyoeleweka mgonjwa wa kwanza wa Ukimwi alipatikana katika kijiji cha kashenye kata kashenye wilaya ya misenyi hapa mkoani Kagera. Ilikisiwa kuwa kuna sehemu zenye maambukizi makubwa ya virusi vya UKIMWI katika maeneo yenye mikusanyiko mingi ikiwemo katika jamii ya wavuvi katika visiwa vya Wilaya ya Muleba na katika mwambao wa ziwa victoria, tatizo la UKIMWI Katika Mkoa wa Kagera linaendelea kupungua kutokana na wanachi kuelewa chanzo na maeneo ambayo ni tete kwa ajili ya maambukizi. Mkoa kwa kutumia gari la sinema umeweza kuhamasisha na kutoa mafunzo kwa njia ya sinema kama ifuatavyo:-
WATU WALIOHUDHURIA KWENYE SINEMA
WILAYA |
2009 |
2010 |
2011 |
Bukoba H/M |
209 |
301 |
271 |
Muleba |
865 |
1,233 |
1,914 |
Karagwe |
720 |
814 |
1,121 |
Misenyi |
1,600 |
2,719 |
2,030 |
Ngara |
1,218 |
899 |
1,300 |
Biharamulo |
1,677 |
1,820 |
537 |
Bukoba H/W |
1,009 |
872 |
988 |
Chato |
1,400 |
1,345 |
2,539 |
Hali hii inadhihirisha yafuatayo: -
Matumizi ya kondomu yamepanda kutokana na kwamba kila mahali sinema ilipoonyeshwa tuliweza kugawa kondom na jumla ya mabokisi 200 yenye kondomu 100 kila moja yaligawiwa kwa wananchi,18,569 wengi wao wakiwa vijana. Aidha, kinamama walijitokeza kwa wingi kuchukulia wenzi wao kondom. sinema ilisababisha wakati wa usiku idadi ya wanaopima afya zao kuongezeka na kuwa kubwa ikilinganishwa na wakati wa mchana hayo yalisemwa na mpimaji kutokana na takwimu alizozipata na kama inavyoonyeshwa hapo chini kwenye jedwali:-
Na. |
HALMASHAURI |
WALIOPIMA |
WALIOKUTWA NA MAAMBUKIZI |
1 |
Bukoba H/M |
672 |
3 |
2 |
Bukoba H/W |
320 |
1 |
3 |
Karagwe |
540 |
2 |
4 |
Chato |
789 |
2 |
5 |
Misenyi |
685 |
6 |
6. |
Muleba |
528 |
8 |
7. |
Ngara |
380 |
2 |
8 |
Biharamulo |
430 |
2 |
Takwimu hizo zinaonyesha kwamba wananchi wengi hupendelea kupima afya zao wakati wa usiku na wako tayari kuchukua majibu yao bila woga pamoja na uhamasishaji kwa njia ya sinema. Mkoa unatumia gari hilo kuhamasisha dhana ya kilimo kwanza ili kuendeleza mapinduzi ya kijani katika mkoa.
Watu wengi wameonyesha kujali maisha yao na kuacha ngono za holela.
Gari la sinema limekuwa kichocheo cha wananchi wengi kubadili tabia na kuacha mila potofu za kujamiiana.
Shule za sekondari 10 zimehamasishwa kwa njia ya sinema ili wanafunzi waache mapenzi wawapo masomoni na kivutio kikubwa ni sinema ya ZAWADI ambayo imewavutia wanafunzi wengi.
Shule za sekondari 40 zimehamasishwa kuhusu janga la UKIMWI na wanafunzi wameanzisha klabu za kupinga na kudhibiti UKIMWI katika shule zao. Aidha, wanafunzi wameanzisha maktaba za kuzuia UKIMWI na kukomesha mimba za utotoni.
Wilaya ya Muleba inaongoza, kwa kuwa na maambukizi makubwa ya UKIMWI kutokana na hali ilivyo huko visiwani. Bado jamii ya wavuvi inaendelea na tatizo la kuwa na ngono za mnada kwamba mwenye fedha nyingi ndiye anayefanya mapenzi na mwanamke mzuri na ambaye ni mgeni katika maeneo ya visiwani. Hii imetokana na utafiti wa shirika lisilo la kiserikali la ADRA na TANESA. WATOTO YATIMA NA WAISHIO KATIKA MAZINGIRA HATARISHI
Mkoa una jumla ya watoto 85,594 ambao wamebainishwa katika Halmashauri za Mkoa wa Kagera, kati yao watoto wa kiume 23,338 na wa kike 23,038 wanahudumiwa na mashirika yasiyo ya kiserikali ambayo husaidia kutoa huduma mbalimbali za kuwaendeleza watoto hao. Mashirika hayo ni TADEPA,MAPEC, WAMATA,KARADEA,SAWAKA,WOMEDA,WVT,HYAWA RC, ELCT, HUMULIZA, MATUMAINI MAPYA UNICEF na mashirika mengi yaliyopo hapa Mkoani. Takwimu hizo ni kwa watoto wanaohudumiwa na mashirika yasiyo ya kiserikali kama zinavyoonyeshwa katika jedwali lifuatalo hapo chini:-
Na |
HALMASHAURI |
ME |
KE |
JUMLA |
1. |
Ngara |
3,118 |
3,062 |
6180 |
2. |
Misenyi |
4,585 |
4,671 |
9256 |
3. |
Karagwe |
3,515 |
3,415 |
6,930 |
4. |
Bukoba H/M |
844 |
1,105 |
1,949 |
5. |
Muleba |
12,905 |
12,455 |
25,360 |
6. |
Chato |
7,600 |
7,252 |
14,852 |
7. |
Bukoba H/W |
9,021 |
8,210 |
17,231 |
8. |
Biharamulo |
2,055 |
1,781 |
3,836 |
|
JUMLA |
43,643 |
41,951 |
85,594 |
Kazi zingine zinazotekelezwa na sekta ya Maendeleo ya Jamii katika mkoa wa Kagera ni pamoja na:-
Kujenga uelewa wa wananchi ili waweze kushiriki shughuli mbalimbali za kujiletea maendeleo yao kwa njia ya kujitegemea na kuwasaidia kupanga mipango inayotekelezeka kwa kutumia mbinu shirikishi ya O & OD.
Kuhamasisha wananchi kujiunga katika vikundi vya kijamii na SACCOS ili kuanzisha na kutekeleza shughuli za uzalishaji mali zenye kuchangia kuinua hali zao za maisha, pamoja na utoaji wa mikopo ya kiuchumi kwa wanawake kupitia mfuko wa maendeleo ya jamii wa wanawake.
Kusaidia jamii jinsi ya kuondokana na mila potofu zinazochangia kuzorotesha maendeleo ya wananchi. Aidha, tatizo la unyanyasaji wa wanawake na watoto linaendelea kufanyiwa kazi na idara ya maendeleo ya Jamii
Wananchi wameelimishwa katika nyanja mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutambua fursa au rasilimali walizo nazo katika kujiletea maendelo yao , pamoja na kutambua vikwazo watumiapo rasilimali hizo(mafunzo ya O&OD yametolewa kwa asilima 98.
Sekta ya maendeleo ya jamii inaendelea kuwa chachu katika kuhamasisha na kuwajengea uwezo wananchi ili waweze kushiriki kikamilifu katika uanzishaji na utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Miradi iliyotekelezwa ni pamoja na ujenzi wa shule za Sekondari za Kata, Barabara za jamii vijijini, mikopo kwa kina mama na vikundi vya wajasiliamali (USHIRIKA), uundaji au uanzishaji wa vikundi vya kijamii (CBOs) pamoja na vikundi vya kinamama.
Utoaji wa mikopo kwa vikundi vya wanawake kwa lengo la kuinua mapato yao na kujiletea maisha bora.
Sekta ya maendeleo ya jamii inaendelea kuhamasisha wananchi kuhusiana na uundaji wa vikundi vya kijamii, na uanzishaji wa SACCOS katika maeneo wanakoishi na sehemu za kazi kama njia ya kuunganisha nguvu zao pamoja na kutumia fursa zilizopo kupitia malengo (2) mawili ya MKUKUTA ili kupambana na umasikini wa kipato na kujiletea maisha bora.
Sekta ya maendeleo mkoani Kagera imekuwa mstali wa mbele kuhamasisha na kuzishauri Halmashauri za Wilaya na manispaa kutoa mchango wa asilimia 5% ya mapato ya Halmashauri katika mfuko wa Maendeleo ya Jamii ili uwe mfuko endelevu, na kuwawezesha kinamama kumiliki mali na kushiriki kuchangia pato la kaya na jamii kwa ujumla.
Aidha sekta ya maendeleo ya jamii kwa kushirikiana na sekta mbalimbali hususan sekta ya Ushirika, Kazi na Vijana hutoa mafunzo kwa wajasiliamali wadogo wadogo kuwapatia elimu na maarifa yatakayowawezesha kuhimili biashara za ushindani katika mazingira yao ya soko huria na utandawazi.
|