JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - OFISI YA MKUU WA MKOA KAGERA
     
 
     
 
 
     
  Maji [ Nyumbani ] au
 
MAJI
 
LENGO::

Kwa kuzingatia Dira ya Taifa, lengo kwa wananchi ni kuwapatia huduma ya maji safi na salama kwa asilimia 90 vijijini na mijini asilimia 100 ifikapo mwaka 2025. Kwa upandewa malengo ya Mellenia ya kuufikia mwaka 2015 huduma ya maji inatarajiwa kuwa asilimia 79 vijijini na asilimia 95 mijini, Malengo ya kati kwa kuzingatia mkakati wa kukuza uchumi na kupunguza umaskini (MKUKUTA II) ni kuongeza huduma ya maji safi na salama hadi asilimia 65 vijijini na asilimia 95 mijini ifikapo mwaka 2015. Tatizo la maji Mkoani Kagera bado ni kubwa kilinganisha na malengo ya Dira ya Taifa. Wastani wa huduma yetu vijijini ni asilimia 55.3, Manispaa ya Bukoba asilimia 76.5 na Makao makuu ya Wilaya za Muleba, Biharamulo,Karagwe na Ngara ni asilimia 65.8 hadi Desemba 2010.

HALI HALISI YA MIRADI YA MAJI MKOANI:

Hadi kufikia Desemba 2010 Miradi yenye Technologia zifuatazo imejengwa na inafanya kazi:

•  Matanki ya kuvuna maji ya mvua - 777

•  Miradi ya maji ya Bomba (bubujiko na msukumo) - 127

•  Miradi ya visima virefu – 281

•  Miradi ya visima vifupi - 1291

•  Vyanzo vya maji vilivyoboreshwa – 842

•  Miradi ya Malambo/Mabwawa – 35

 

Upatikanaji wa huduma ya maji kwa wilaya za Mkoa wa Kagera ni kama ifuatavyo:-

Na

Wilaya

Asilimia ya upatikanaji wa Maji

Idadi ya mifuko ya Maji

Mifuko ya Maji Tshs:

Maelezo

 

 

Vijijini

Mjini

1.

Bukoba (M)

56

76.5

 

 

 

2.

Bukoba (V)

55

 

29

8,100,000

 

3.

Biharamulo

48.5

62.2

49

24,564,350

 

4.

Chato

44

-

52

13,560,350

Hakuna Mamlaka ya maji mji mkuu wa Wilaya

5.

Karagwe

48

48

86

15,000,000

 

6.

Missenyi

57

-

72

3,920,000

Hakuna Mamlaka ya maji mji mkuu wa Wilaya

7.

Muleba

62.1

65

39

8,943,465

 

8.

Ngara

72

88

68

9,263,000

 

JUMLA

 

53.5

 

65.8

 

395

 

83,351,165

 

 

 

 

 
 

 

 
 
 

 

 
 
 
   

Eng. Avitus Exavery-Mhandisi wa maji Sekretarieti ya Mkoa

MAFANIKIO

Upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama kwa wananchi wa mkoa wa Kagera waishio vijijini umefikia wastani wa asilimia 55.3. na Manispaa ya Bukoba asilimia 76.5. Jitihada hizi zimepatikana kutokana na fedha za serikali, wahisani na michango ya wananchi.

•  Kuanzisha Kamati za Maji za Vijiji hadi kufikia 483 (asilimia 64.6) kati ya vijiji 748. Idadi ya mifuko ya maji imefikia 395 yenye jumla ya Tshs, 83,351,165.

•  Kuunda sheria ndogo ndogo za Halmashauri ili kulinda uharibifu wa vyanzo vya maji na mazingira.

•  Kusajiri vyombo huru vya watumiaji maji (COWSOs).

•  Kuanzisha Bodi za maji za miji mikuu ya wilaya katika miji ya Biharamulo, Ngara, Muleba na Karagwe.

CHANGAMOTO:

Uharibifu wa vyanzo vya maji na mazingira hususan uchomaji moto bado ni mkubwa.

•  Uharibifu wa Miradi mingi mikubwa ya bomba inayoendeshwa na mitambo kutokana na jamii kushindwa kupata fedha za uendeshaji na matengenezo.

•  Ukosefu wa ulipiaji wa maji mijini ambalo ni tatizo kubwa kwa baadhi ya Taasisi kwa wakati mwafaka

Ukosefu wa vipuri vya kufanyia marekebisho ya miradi ya maji kwa wakati mwafaka.

MIKAKATI YA KUKABILIANA NA CHANGAMOTO:

•  Matumizi ya sheria ndogo ndogo za hifadhi ya vyanzo vya maji yametiliwa mkazo Aidha upandaji wa miti rafiki wa maji na kukata miti ambayo hufyonza maji mengi kama Mikalitusi na kusababisha vyanzo vya maji kukauka unaendelea.

• Uhamasishaji wa Kamati za Maji na vikundi vya watumiaji maji ikiwa ni pamoja na kutunisha mifuko ya maji kwa shughuli hizo unafanyika.

•  Mamlaka za maji kwa kushirikiana na viongozi wa Mkoa na Wilaya hali hii imeanza kubadilika kwa baadhi ya Taasisi kwa kulipia malimbikizo ya madeni yao .

•  Tunahimiza ujenzi wa miradi yenye Technologia nyepesi kama uvunaji wa maji ya mvua, uchakavu wa miundo mbinu mijini unaosababisha upotevu wa maji mengi na kusababisha gharama kubwa za uendeshaji na matengenezo. Jitihada zinafanywa kulekebisha miundo mbinu kwa fedha za Serikali na Wahisani.

•  Serikali inatekeleza Programu ya maji ambapo utekelezaji wake kwa upande wa vijijini umefikia hatua ya kujenga miundombinu ya maji kwenye vijiji kumi vya awali kwa kila hHalmashauri ya Wilaya.

Na kwa upande wa mjini Mhandisi Mshauri atakayefanya utafiti na kusanifu miradi ya maji kwenye miji mikuu ya Wilaya za Mkoa wa Kagera yuko kwenye hatua za mwisho za kupatikana kwake.

 

 
 
 

 

 

 

 
 
 
 
Maji [ Nyumbani ] au
Rudi juu
 
     
Copyright © 2008 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera, BUKOBA, TEL: 028 - 2220215/17, FAX: 028-2752184