JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - OFISI YA MKUU WA MKOA KAGERA
     
 
     
 
 
     
MAZINGIRA
 
[ Maliasili ] Mazingira [ Nyumbani ] au
 
 
 
UTANGULIZI
 

Sera ya sheria ya usimamizi wa Mazingira Na. 20 ya mwaka 2004 imeendelea kutekelezwa katika mkoa wa Kagera.Katika utekelezaji wa sera na sheria,Mkoa uliandaa mpango shirikishi jamii wa hifadhi ya mazingira. Mpango huu unaainisha uhusiano uliopo kati ya uharibifu wa mazingira na umaskini uliokithiri kwa sababu maliasili kama vile ardhi,misitu na vyanzo vya maji;ambazo hutumika katika uzalishaji huharibiwa na kushindwa kutoa tija inayokusudiwa na hivyo kukwamisha juhudi za wananchi kufikia lengo la maisha bora kama ilivyo katika Dira ya Taifa ya maendeleo (2025)

 
 
 
 
HIFADHI YA MAZINGIRA YA ZIWA VICTORIA
 

Mikakakti ya utekelezaji wa mpango wa hifadhi ya mazingira ya ziwa vixtoria iliyotekelezwa katika kipindi hiki na kutoa Elimu kwa wadau wa ziwa Victoria kwa kupitia semina na makongamano ya wavuvi, viongozi wa sErikali,Viongozi wa asasi zisizo za Kiserikali,wamiliki wa vyombo vya usafiri wa maji,na jamii iliyo kando kando ya ziwa Victoria. Taasisi ya uangalizi na uendelezaji wa ziwa Victoria (LVFO) kwa kushirikiana na wadau wengine wa ziwa Victoria wamesaidia kutekeleza mkakati kabambe wa Mkoa wa kuunda na kuwezesha vikundi vya ulinzi wa Rasilimali na usimamizi shirikishi wa Rasilimali ikiwa ni pamoja na dhana ya ujasiriamali na kuinua kipato cha wananchi kwa kutumia ziwa Victoria bila kuathiri mazingira.

 
 
 
UPANDAJI NA UTUNZAJI WA MITI
 

Upandaji wa miti umefanyika kwa kila wilaya ili kutekeleza malengo waliyojiwekea na kwa kuzingatia lengo la kitaifa la kupanda miti 1,500,000 kwa kila wilaya nchini. Katika kipindi hiki kuishia mwezi machi 2008 wilaya za ngara na muleba ndizo zilifanya vizuri zaidi katika utekelezaji wa mkakati wa Mkoani wa upandaji na utunzaji wa miti.

Aidha serikali ya mkoa kwa kushirikiana na Halmashauri za wilaya ilifanya shughuli za doria kwa ajili ya kudhibiti uvamizi na uharibifu wa misitu ya Hifadhi.Zilifanyika pia doria katika mapori ya akiba ya Burigi,Biharamulo na Nyantakala ili kuzuia uwindaji haramu na uchungaji ndani ya mapori haya.

 
MATUMIZI YA MAJIKO SANIFU NA NISHATI MBADALA
 

Mkoa kwa kushirikiana na mashirika yasiyo ya kiserikali unaendelea kuhamasisha wananchi juu ya matmizi ya nishati mbadala kama vile jua (solar power),biogas na majiko sanifu.Katika kipindi hiki uhamasishaji katika wilaya za chato,Muleba,Biharamulo,karagwe,Missenyi na Ngara kwa kutumia timu za wawezeshaji jamii za kata na wilaya.Lengo la mkoa ni kupunguza matumizi ya mkaa kwa asilimia 25 ifikapo mwaka 2010,maana uchomajimkaa na ukataji wa kuni ni miongoni mwa vyanzo vya uharibifu wa mazingira.

 

.

 
 
 
UCHOMAJI MOTO MISITU
 

Mkakati wa mkoa wa kuhamasisha wananchi kuhusu kupiga vita uchomaji moto misitu ovyo umefanikiwa kwa kiasi kikubwa.Matukio ya uchomaji moto misitu yamepungua kutoka 367 mwaka 2006 hadi 124 mwaka huu.Mafanikio haya kwa kiasi kikubwa yametokana:-

Kuanza kutumika kwa sheria ndogo za kutunza na kuhifadhi mazingira pamoja na kudhibiti uchomaji moto ovyo.

-Vijiji vyote vilivyo kando kando ya misitu kushiriki katika mchakato wa mpango shirikishi jamii wa hifadhi ya mazingira(PFM).

Suala la uchomaji misitu ovyo kufanywa kuwa agenda ya kudumu katika mikutano yote ya hadhara ya viongozi wa wa serikali pamoja na viongozi wa kisiasa mikoani.

_Kukamatwa kwa wahalifu wa uchomaji moto ovyo na kukamatwa kisheria.

.Kuv
 
 
 
 
 
 
HIFADHI YA ARDHI NA VYANZO VYA MAJI
 

Mkakati wa Mkoa wa kutekeleza programu ya Hifadhi ya Mazingira ya ardhi na vyanzo vya maji umetekelezwa kwa kufanya shughuli(activities) zote zilizokuwa zimepangwa kwa kipindi cha kuishia mwezi Machi,2008.Wilaya za Bukoba,Karagwe,na Missenyi kwa kushirikiana na shirika lisilo la kiserikali la SCC Vi-Agroferestry na wilaya ya Ngara kupanda mashamba ya mfano katika kila kata.Aidha ,mafunzo kwa vikundi yameendelea kutolewa kwa kutumia mashamba darasa.

Uhamasishaji wa kutekeleza mpango wa Hifadhi ya ardhi na vyanzo vya maji pamoja na shughuli za kilimo mseto umefanikiwa katika wilaya zote kwa kushirikina na mashirika na wadau mbalimbali.Wadau hao ni TADEPA,KADETFU, CHEMA,REDESO,FAIDERS,KADET,KAWEF,OBUHANGWA MDA na Gugu maji Kassambya.Uharibifu wa mazingira utokanao na uvamizi wa kukakamilisha program ya kuainisha na kutenga maeneo ya vyanzo vya maji na maeneo yafaayokwa ufugaji.

 
 
 
HIFADHI YA MAZINGIRA YA MIJI NA UTUPAJI TAKA.
 

Katika kuadhimisha siku ya mazingira Duniani mwaka huu,kila wilaya iliombwa kuandaa program ya maadhimisho haya.Miongoni mwa shughuli zilizobainishwa na wilaya zote ni kusafisha mitaro,kufanya usafi katika maeneo ya makazi pamoja na kuhimiza utumiaji wa mashimo au vyombo vya kutupia taka za majumbani na maofisini.Programu hizi za wilaya zimeunganishwa na kupata programu ya Mkoa iliyowasilishwa katika katika Ofisi ya Makamu wa Rais(mazingira) kwa aili ya utekelezaji.

 
 
 
CHANGAMOTO YA UHIFADHI WA MAZINGIRA.
 

Pamoja na utekelezaji mzuri wa programu ya Hifadhi ya mazingira kama inavyoonekana katika Taarifa,bado kuna mapungufu yaliyojitokeza kama changamoto katika kufikia malengo ya programu.

(i)Wachimbaji wadogo wadogo bado wanaendelea kuharibu kuharibu mazingira kwa uchimbaji holela wa madini katika vyanzo vya maji ndani ya pori la matabe.

(ii)Uchafuzi wamazingira unatokana na taka ngumu pamoja na plastiki bado unaendelea pamoja na jitihada kubwa iliyofanywa na wakuu wa wilaya kupitia miongozo iliyotolewa na ofisi ya makamu wa Rais kitengo cha mazingira .

(iii)Baadhi ya wilaya hazina jaa maalumu la utupaji taka(dampo)na hivyo kusababisha utupaji ovyo wa taka.Hali hii ni chanzo chanzo cha kupata magonjwa ya mlipuko.

(iv)Hali ya mazingira katika Bandari ya Kemondo na Bukoba Port siyo ya kuridhisha.Pamoja Ufuatiliaji uliofanywa na Halmashauri husika hamna shughuli yoyote ya utunzaji wa mazingira imefanyika hadi sasa.

(v)Shughuli za kilimo bado zinafanyika kwenye miteremko ya milima ,mabondeni na kwenye vyanzo vya maji hasa katika wilaya za Biharamulo ,Muleba,Ngara na Karagwe.

(vi)pamoja na kwamba takwimu zinaonyesha kupungua kwa tatizo la uchomaji moto,bado hali si ya kujipongeza sana.

 
 
 
 
 

 

i
 
 
 
     
     
 
 
 
     
Copyright © 2008 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera, BUKOBA, TEL: 028 - 2220215/17, FAX: 028-2752184