• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

TEHAMA

LENGO LA KITENGO CHA TEHAMA

Kuwezesha utoaji wa ushauri wa kitaalam katika sekta za uchumi na uzalishaji kwenye Halmashauri

Sehemu hii inafanya kazi zifuatazo:-

  • Kushauri Menejimenti juu ya mausala ya TEHAMA na utekelezaji wa e-government/serikali mtandao
  • Kufuatilia na kusaidia Mamlaka za Serikali za Mitaa juu ya masuala TEHAMA
  • Kutoa msaada wa kiufundi katika matumizi ya vyombo vya kielektroniki
  • Kushauri Menejimenti juu ya utekelezaji wa sera ya TEHAMA

Kwa kuzingatia umuhimu wa TEHAMA na lengo la serikali la kuwa na serikali mtandao, Mkoa wa Kagera ni miongoni mwa taasisi za serikali ambao unafanya vizuri katika eneo la TEHAMA.

Teknolojia ya Habari na Mawasiliano Mkoani Kagera ni ya kuridhisha kwa sasa.

MAWASILIANO YA SIMU

Kampuni kongwe ya TTCL ndio inayotoa huduma za mawasiliano ya njia ya simu katika ofisi zote za serikali na mashirika Mkoani Kagera. Makampuni mengine ya simu za mkononi yametawanyika vizuri hadi katika baadhi ya vijiji na hivyo kufanya mawasiliano kuwa rahisi zaidi. Hali hiyo imewasaidia wakulima kujua bei halali ya soko la mjini kwa mazao yao na hivyo kuondoa adha ya kuibiwa na wafanyabiashara kwa kisingizio kuwa soko la bidhaa husika ni mbaya.

TELE-CENTERS

Mkoa una vituo viwili hadi sasa vinavyotoa huduma ya TEHAMA vijijini. Kituo kimoja kipo wilaya ya Bukoba vijijini katika kijiji cha Kibegwe kata ya Bugabo, na kingine kipo katika wilaya ya Ngara. Vituo hivyo vimekuwa vikitoa huduma nzuri kwa wanavijiji wa maeneo husika, ingawa vimekuwa havitoi huduma ipasavyo kutokana na mwamko duni wa wanavijiji katika matumizi ya TEHAMA.

VITUO VYA REDIO

Kutokana na mabadilko ya sera za habari na mawasiliano ambapo vituo binafsi vya radio vimeruhusiwa kuanzishwa, mkoa wa Kagera sasa una vituo vitano (5) vya radio. Vituo hivyo ni

Kasibante FM Redio iliyoko Bukoba

Radio Vision iliyoko Bukoba

Karagwe FM iliyoko Karagwe

Redio Fadeko iliyoko Karagwe

Radio Kwizera iliyoko Ngara

Ofisi ya Mkuu wa Mkoa imejenga miundombinu ya TEHAMA iliyo bora kwa ajili ya kuwa na serikali -mtandao .Aidha Ofisi nyingi hapa Mkoani hutumia teknolojia ya kompyuta katika kufanikisha shughuli za kila siku.

Hadi kufikia Septemba, 2013 mifumo mbalimbali ya kompyuta zaidi ya ishirini imefungwa katika Ofisi za serikali mkoani Kagera ili kurahisisha utendaji kazi wake. Ofisi moja ya mkuu wa wilaya ya Muleba imefungiwa miundombinu ya intaneti na hivyo kurahisisha mawasiliano kati ya Ofisi ya mkuu wa Mkoa na ofisi hizo. Aidha, mkoa unaendelea na juhudi za kuhakikisha kila Ofisi ya mkuu wa wilaya inafungiwa miundombinu ya intaneti ili kurahisisha mawasiliano.

Halmashauri za Ngara, Biharamulo, Kyerwa na Bukoba hazina miundombinu ya TEHAMA iliyo bora hadi sasa isipokuwa Manispaa ya Bukoba na halmashauri za Karagwe na Misenyi. Juhudi nyingi zinafanywa ili kujenga miundombinu hiyo kabla ya mwaka 2015 kwa lengo la kuharakisha lengo la serikali la kuwa na Serikali -Mtandao.

HUDUMA YA INTANETI

Huduma ya intaneti Mkoani Kagera hutolewa na makampuni mbalimbali. Kampuni kongwe ya TTCL ndiyo inayotoa huduma ya intaneti katika ofisi nyingi za serikali na mashirika. Aidha, makampuni ya simu za mikononi kama Vodacom, Tigo, Airtel na Zantel yanatoa huduma muhimu ya intaneti kupitia simu za mikononi na "moderm". Zipo pia baadhi ya ofisi ambazo hutumia makampuni mengine kwa ajili ya kupata intaneti. Makampuni hayo ni pamoja Simbanet ya jijini Dar es Salaam.

MKONGO WA TAIFA

Mkongo wa Taifa ambao tayari umefika mkoani Kagera, umeweza kuongeza ufanisi wa huduma ya intaneti kwa kiwango kikubwa. Hadi sasa kampuni ya simu ya TTCL imeweza kutoa huduma bora zaidi za intaneti baada ya mkongo wa Taifa kuanza kufanya kazi hapa mkoani Kagera. Uwepo wa mkongo wa Taifa umepunguza gharama za intaneti katika ofisi za Serikali na pia umeongeza watumiaji wa intaneti katika Mkoa wa Kagera. Baadhi ya mabenki Mkoani Kagera, ofisi za TRA, Ofisi ya madini, NSSF zimeungwanishwa kwenye mkongo kupitia TTCL.

MIFUMO YA KOMPYUTA INAYOTUMIKA HADI SASA MKOANI KAGERA

Hadi kufikia Septembal, 2013 ofisi ya mkuu wa mkoa wa Kagera, Halmashauri za mkoa na manispaa ya Bukoba zimefungiwa mifumo ifuatayo;

Epicor--Mfumo huu hutumika katika kuandaa na kutoa malipo. Mfumo huu umesaidia sana na umepunguza hoja za ukaguzi kwa kiwango kikubwa. Mfumo huu umeunganishwa kwa kutumia mkongo wa Taifa.

SBAS--Huu ni mfumo kwa ajili ya kuandaa mipango ya serikali kuu.Bajeti ya Sekretariet ya Mkoa huandaliwa kwa kutumia mfumo huu.

PlanRep--Mfumo huu ni sawa na SBAS, tofauti ya mifumo hii miwili ni kuwa mfumo huu wa PlanRep hutumiwa na Halmashauri pamoja na Manispaa wakati wa kuandaa bajeti za Mamlaka ya Serikali za Mitaa.

CDR na CFR--Hii ni mifumo inayotumika kutolea taarifa za miradi ya maendeleo katika ngazi za Mamlaka ya Serikali za Mitaa.

ETR--Huu ni mfumo unaotumika kutunza takwimu za wagonjwa wa kifua kikuu

LGHRIS-Mfumo huu unatumika katika kutunza taarifa za watumishi na unatumika katika ngazi ya mkoa na halmashauri.

Lawson-Huu ni mfumo unaotumika katika mishahara, kwa kutumia mfumo huu, serikali imeondoa tatizo la mishahara hewa, kuchelewa kwa stahili za watumishi n.k.

LGMD- Mfumo huu unatumika katika kukusanya na kutunza takwimu katika ngazi ya halmashauri. Takwimu hizi ndizo hutumika katika kuandaa mipango ya halmashauri.

MVC Database-Mfumo huu hutumika katika kutunza taarifa za watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi katika ngazi ya halmashauri.

Aidha, ipo mifumo mingine ambayo si rahisi kuiweka hapa ambayo inapatikana katika baadhi ya halmashauri.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa